Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kisukari Nawashukuru kwa dhati kwa makala “Kuishi na Kisukari.” (Mei 8, 2003) Nimeugua kisukari tangu nilipokuwa na umri wa miaka minne. Sikuzote nilifikiri kwamba singeweza kufunga ndoa au kuingia katika huduma ya wakati wote, lakini makala hizo zilinipa tumaini. Sasa, nikiwa na umri wa miaka 17, nina mradi wa kuwa mtumishi wa wakati wote na nitajitahidi niwezavyo kuufikia.

T. A., Japan

Nawashukuru kwa dokezo muhimu mlilotoa kwamba watu wa familia na marafiki hawapaswi kuwachochea watu wenye kisukari wale vyakula visivyowafaa. Mimi huona ugumu kupikia familia yangu chakula na nisiweze kukila. Huenda watu wasio na kisukari wakaona jambo hilo kuwa dogo, lakini ninawahakikishia kwamba si jambo dogo!

V. N., Italia

Mimi ni muuguzi na mwalimu. Muhula ujao, nitawafundisha wanafunzi kuhusu kisukari. Picha iliyoko kwenye ukurasa wa 8 na 9 inaeleweka kwa urahisi, na nitaitumia kufundisha. Asanteni kwa kuandika mambo ya kitiba kwa njia rahisi.

C. B., Ufaransa

Asanteni kwa makala zinazohusu kisukari. Mimi sina ugonjwa huo, lakini dadangu mwenye umri wa miaka 14 anao. Sasa ninaelewa matatizo yake. Ni kweli kwamba ninahitaji kujinyima mambo fulani kwa ajili yake, lakini kufanya hivyo si vigumu kama kuishi na kisukari!

E.D.M., Italia

Mama yangu ameugua kisukari kwa miaka mitano. Mara nyingi mimi huwa na wasiwasi kuhusu afya yake kwa sababu ninaishi mbali sana naye. Ninanuia kumtumia gazeti hilo kwani linaweza kumsaidia wakati sipo.

R. W., Indonesia

Kujeruhiwa Nilifurahia kusoma makala “Jinsi Maisha Yangu Yalivyobadilika Nilipojeruhiwa.” (Aprili 22, 2003) Makala hiyo inanisaidia nikabiliane na jeraha langu la mgongo la zaidi ya miaka 30. Nilikabili mengi ya matatizo ambayo Ndugu Stanley Ombeva alikuwa nayo. Ninafarijiwa kujua kwamba Neno la Mungu linaweza kumsaidia mtu amtegemee Yehova.

G. G., Marekani

Nilichochewa sana na jinsi Ndugu Ombeva alivyosimulia waziwazi jinsi alivyoona matatizo yake. Nilitambua kwamba matatizo yangu ni madogo sana yakilinganishwa na yake. Makala hiyo ilinisaidia kuthamini baraka zangu.

S. C., Kanada

Ajabu! Ndivyo ninavyoweza kuielezea makala hiyo. Nilisoma makala yote mara moja. Nilichochewa kuona jinsi Maandiko yalivyomsaidia sana Ndugu Ombeva alipoyahitaji sana. Hiyo itanisaidia niwe na huruma ninapowasaidia wengine.

R. G., Marekani

Nilitiwa moyo kujua kwamba hata Mkristo ambaye ni mzee wa kutaniko anaweza kukasirika na nilitambua kwamba inachukua muda kukabiliana na hali kama hiyo. Ndugu Ombeva alisema kwamba hata alipokuwa na matatizo mengi zaidi, hakuacha kuhubiri. Nimechochewa kufanya vivyo hivyo.

M. K., Japan

Nilipokuwa mdogo nilianguka mara nyingi na sasa ninaumia kwa sababu hiyo. Mimi huwa na maumivu kila wakati, hushindwa kutembea, na huwa dhaifu. Mimi hufadhaika kwa sababu siwezi kutimiza mengi katika huduma ya Kikristo. Lakini nilifaidika niliposoma jinsi Ndugu Ombeva alivyoshughulikia tatizo lake. Asanteni sana!

E. E., Marekani