Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Maadili Nilishangaa niliposoma fungu la kwanza katika makala ya pili ya mfululizo “Kwa Nini Maadili Yanabadilika?” (Juni 8, 2003) Lilisema: “Zawadi kubwa sana ambayo wazazi wanaweza kuwapatia watoto wao ni upendo wa kweli na maadili ambayo wanayafuata wala si kuyafundisha tu.” Watoto na watu wazima wakitendeana kana kwamba wana haki ya kupokea upendo kutoka kwa mmoja na yule mwingine, maadili yatazorota kabisa.

K. B., Marekani

“Amkeni!” linajibu: Maneno “upendo wa kweli” yalitumiwa kumaanisha kwamba wazazi hawapaswi kuwa vigeugeu wanapowapenda watoto wao, kwamba hawapaswi kuacha kuwapenda wakati wanapokosea au kuwapenda tu wasipokosea.—Waefeso 6:4; Wakolosai 3:21.

Makala ya mwisho iliandikwa vizuri sana. Habari hiyo ni rahisi kuelewa, imeandikwa kwa utaratibu, na inatia moyo sana. Ina picha maridadi. Asanteni kwa makala kama hizo zenye kufariji.

M. P., Marekani

Maji Asanteni sana kwa makala “Maji Ni Muhimu kwa Uhai.” (Juni 8, 2003) Makala hiyo ilinukuu mtaalamu wa tatizo la kunenepa kupita kiasi aliyesema kwamba watu wenye afya wanapaswa kunywa lita mbili au lita mbili u nusu kila siku. Hata hivyo, moyo au figo ya mtu ikishindwa kufanya kazi, madaktari huwaambia wagonjwa wasinywe maji mengi sana.

T. A., Japan

“Amkeni!” linajibu: Madokezo kuhusu jambo hilo yanatofautiana. Wataalamu wengine husema kwamba watu hawapaswi kunywa maji mengi ikiwa wana matatizo fulani ya afya. Inafaa mtu amuulize daktari wake kuhusu jambo hilo.

Kushuka Moyo Baada ya Kujifungua Mimi ni mama, na nina msichana mchanga mwenye umri wa mwaka mmoja ninayempenda sana. Sijawahi kuhisi mkono wa Yehova ukiwa karibu nami kama nilivyohisi nilipofungua Amkeni! na kusoma makala “Kuelewa Mshuko wa Moyo Baada ya Kujifungua.” (Juni 8, 2003) Sina maneno ya kutosha kuwashukuru kwa ajili ya makala hiyo. Nashukuru kuwa miongoni mwa watu wanaojali hisia za kila mmoja. Asanteni tena na tena!

M. G., Hispania

Fumbo la Kujaza Maneno Asanteni kwa Amkeni! la Juni 8, 2003. Nilipata jambo ninalothamini sana, yaani fumbo la kujaza maneno! Nimekuwa Shahidi wa Yehova kwa miaka minne hivi, na kwa muda huo wote nimekuwa nikijaza mafumbo yote ambayo yamechapishwa. Ni njia nzuri sana ya kujua Maandiko. Endeleeni kufanya kazi hiyo nzuri. Natazamia kujaza mafumbo ya wakati ujao.

K. G., Marekani

“Amkeni!” linaeleza: Maswali ya Biblia katika makala “Je, Wajua?” huchapishwa katika magazeti ya “Amkeni!” ya lugha ambazo hazina fumbo la kujaza maneno.

Hisi Asanteni kwa mfululizo wa makala “Hisi Zenye Kustaajabisha—Je, Unazithamini?” (Machi 8, 2003) Hisi hutusaidia sana kufurahia uhai na mazingira yetu. Makala kama hizo hutusaidia tumpende Mungu zaidi. Asanteni kwa kuzichapisha.

J. N., Burundi

Vitu vya Kimwili Ningependa kuwashukuru kwa ajili ya makala “Maoni ya Biblia: Inamaanisha Nini Kupenda Vitu vya Kimwili?” (Aprili 8, 2003) Ni kweli kwamba watu wengi leo wanatamani sana kuwa na vitu vya kimwili, na kwa kusikitisha, tatizo hilo linaweza kuwaathiri hata Wakristo. Makala hiyo ilinisaidia kufahamu maana ya kupenda vitu vya kimwili na jinsi ya kuepuka tatizo hilo. Sasa nitafanya kila ninaloweza ili nizingatie mambo ya kiroho badala ya vitu vya kimwili. Asanteni sana kwa kuchapisha makala hiyo yenye kuarifu!

Z. K., Urusi