Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Sala Yangu Ilijibiwa”

“Sala Yangu Ilijibiwa”

“Sala Yangu Ilijibiwa”

Hivyo ndivyo mama ya mvulana mwenye umri wa miaka tisa alivyosema kuhusu kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu kilipotolewa kwenye kusanyiko la wilaya la Mashahidi wa Yehova huko Ireland. “Nilitiririkwa na machozi!” akasema. “Ilikuwa baraka kwani juma moja tu lililopita sikujua nitajifunza nini na mwanangu.

“Nilikuwa nimesali kwa Yehova anisaidie kumfundisha kweli za Biblia zenye kina kwa njia rahisi na yenye kupendeza, lakini sikujua nianzie wapi. Kwa hiyo nilipopokea kitabu hicho maridadi chenye picha nyingi, sala yangu ilijibiwa.”

Mama ya watoto watano huko California, Marekani, aliandika hivi: “Tulipokuwa tukirudi hotelini kutoka kwenye kusanyiko, niliwapata watoto wangu watatu wachanga zaidi wakisoma, wakitazama, na kuzungumzia mambo yaliyowasisimua katika kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu.”

Aliongeza hivi: “Shangwe niliyohisi nilipopokea zawadi hiyo kutoka kwa Yehova haina kifani—ni kama shangwe inayopatikana mtoto anapozaliwa, wakati wa arusi, ubatizo, au mtu anapopata pendeleo kutoka kwa Muumba wa ulimwengu mzima. Nyakati nyingine machozi yetu ya shangwe humwonyesha Baba yetu mwenye upendo, Yehova, mambo tusiyoweza kueleza kwa maneno.”

Huenda wewe pia utahisi hivyo unaposoma kitabu hicho maridadi chenye picha nyingi cha kurasa 256 zenye ukubwa wa kurasa za gazeti hili. Unaweza kuomba nakala kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na uitume ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.