Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kutembea Pamoja na Mungu Huleta Baraka Sasa na Milele”

“Kutembea Pamoja na Mungu Huleta Baraka Sasa na Milele”

“Kutembea Pamoja na Mungu Huleta Baraka Sasa na Milele”

MARA nyingi watu husema kwamba maisha ni kama safari. Hata hivyo, je, wewe huhisi, kama wengi wanavyohisi, kwamba maisha yako hayana kusudi? Tunaishi katika ulimwengu wenye magumu mengi. Kadiri jeuri na ukosefu wa maadili unavyozidi, huenda tukahisi kuwa tumesongwa na mambo yanayopita uwezo wetu. Katika nyakati za misukosuko kama hiyo, tunawezaje kuendelea kusimama imara? Tunawezaje kuendelea kutembea katika njia inayofaa?

Biblia ina majibu mazuri na yenye kufariji. Inaonyesha kwamba tuna pendeleo zuri ajabu, yaani, tunaweza kutembea pamoja na Mungu. Huenda wengine wakadhihaki wazo hilo. Mwanadamu anawezaje kutembea pamoja na Muumba wa ulimwengu? Biblia inaonyesha kwamba inawezekana kufanya hivyo. Kwa hakika, kutembea pamoja na Mungu humwezesha mtu kuishi maisha bora na yenye furaha zaidi katika ulimwengu huu wenye taabu. Hata hivyo, kutembea pamoja na Mungu kunahusisha nini? Na mtu anaweza kupata baraka gani kwa kufanya hivyo?

Maswali hayo yatajibiwa katika hotuba ya kusisimua yenye kichwa: “Kutembea Pamoja na Mungu Huleta Baraka Sasa na Milele.” Hotuba hiyo ya watu wote itatolewa katika makusanyiko ya wilaya ya Mashahidi wa Yehova yatakayoanza mwezi huu. Mamia ya makusanyiko hayo yatafanywa ulimwenguni pote. Ili kujua kusanyiko litakalofanywa mahali unapoweza kuhudhuria, wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lako au uwaandikie wachapishaji wa gazeti hili. Gazeti la Mnara wa Mlinzi, toleo la Machi 1, 2004, lina orodha ya mahali pa makusanyiko hayo nchini Burundi, Kongo (Kinshasa), Kenya, Rwanda, Tanzania, na Uganda.