Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Karibuni Kwenye Kusanyiko la Wilaya la “Tembea Pamoja na MUNGU”

Karibuni Kwenye Kusanyiko la Wilaya la “Tembea Pamoja na MUNGU”

Karibuni Kwenye Kusanyiko la Wilaya la “Tembea Pamoja na MUNGU”

▪ Mamilioni ya watu watahudhuria kusanyiko hilo katika sehemu nyingi ulimwenguni pote. Makusanyiko ya kwanza kati ya makusanyiko 74 ya siku tatu katika Afrika Mashariki na Kongo yatafanywa Agosti 6-8, na la mwisho litafanywa Septemba 18-19. Makusanyiko 47 yatafanywa katika Kiswahili. Huenda mojawapo ya makusanyiko hayo ya siku tatu litafanywa katika jiji lililo karibu nawe. Kwa kawaida, makusanyiko hayo hufanywa kuanzia Ijumaa hadi Jumapili.

Katika sehemu nyingi, programu itaanza kwa muziki saa 3:30 kila siku. Kichwa cha siku ya Ijumaa ni “Hii Ndiyo Njia. Tembeeni Ndani Yake.” Baada ya hotuba yenye kichwa, “Tumekusanyika Ili Yehova Atufundishe Njia Zake,” kutakuwa na sehemu ya kuwahoji wale ambao wamekuwa wakitembea kwa uaminifu pamoja na Mungu. Baada ya hotuba zenye kichwa “Endeleeni Kuthibitisha Ninyi Wenyewe Jinsi Mlivyo” na “Neno la Mungu na Liongoze Hatua Zako Kila Siku,” kipindi cha asubuhi kitamalizika kwa hotuba ya msingi yenye kichwa, “Tembea Pamoja na Mungu Nyakati za Misukosuko.”

Ijumaa alasiri kutakuwa na mfululizo wa hotuba tatu zenye kichwa, “Unabii wa Hosea Hutusaidia Kutembea Pamoja na Mungu.” Baada ya hotuba hizo kutakuwa na hotuba zifuatazo, “Usitenganishe ‘Kile Ambacho Mungu Ameunganisha’” na “Kuheshimu Mikusanyiko Yetu Mitakatifu.” Hotuba ya mwisho siku hiyo yenye kichwa, “Habari Njema kwa Watu wa Mataifa Yote” itatutia moyo kuwahubiria watu wa lugha zote habari njema.

Kichwa cha Jumamosi ni “Endeleeni Kuangalia Sana Jinsi Mnavyotembea.” Mfululizo wa hotuba zitakazotolewa asubuhi hiyo wenye kichwa, “Wahudumu Wanaofanya Maendeleo,” utakuwa na mapendekezo mengine kuhusu jinsi ya kuwahubiria watu wanaozungumza lugha nyingine. Programu ya asubuhi hiyo itamalizika kwa hotuba muhimu yenye kichwa, “Kutembea Pamoja na Yehova kwa Mapatano,” kisha wale wanaostahili watapata nafasi ya kubatizwa.

Hotuba za Jumamosi alasiri zatia ndani “Epuka ‘Sababu Yoyote ya Kukwaza’” na “Utendaji Unaojenga na Kuburudisha.” Kisha, hotuba zitakazofuata, “Yehova Ni Mchungaji Wetu,” “Kununua Wakati Unaofaa,” na “Kutembea Katika Njia ya Nuru Inayozidi Kuongezeka,” zitakuwa na mahojiano yenye kutia moyo. Kipindi hicho kitamalizika kwa hotuba muhimu yenye kichwa “‘Endeleeni Kukesha’—Saa ya Hukumu Imefika.”

Kichwa cha programu ya Jumapili, “Endelee- ni Kutembea Katika Kweli,” kitakaziwa katika hotuba yenye kichwa “Enyi Vijana, Tembeeni Katika Njia ya Uadilifu.” Baada ya hotuba hiyo kutakuwa na drama ya nyakati za Biblia kuhusu huduma ya mtume Paulo. Kisha kutakuwa na hotuba inayokazia mambo tunayoweza kujifunza kutokana na drama hiyo. Alasiri, kutakuwa na hotuba ya watu wote yenye kichwa, “Kutembea Pamoja na Mungu Huleta Baraka Sasa na Milele.”

Ili kujua mahali ambapo kusanyiko la kwenu litafanywa, unaweza kupata habari katika Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova au uwaandikie wachapishaji wa gazeti hili. Katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, kuna orodha ya mahali ambapo makusanyiko yote yatafanywa nchini Burundi, Kenya, Kongo (Kinshasa), Rwanda, Tanzania, na Uganda.