Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kubalehe Ni Kipindi Kizuri na Kigumu

Kubalehe Ni Kipindi Kizuri na Kigumu

Kubalehe Ni Kipindi Kizuri na Kigumu

KUBALEHE kunaweza kuwa kipindi kizuri sana maishani. Vijana wengi hufurahia kipindi hicho. Na watu wazima wengi wanakumbuka jinsi walivyofurahia miaka yao ya ujana.

Wakati huohuo, ni lazima tutambue kwamba tunaishi katika “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1) Hilo limewaongezea vijana mkazo mwingi kuliko ule ambao vijana walikabili zamani. Huenda ndiyo sababu Sabrina Solin Weill, mhariri mkuu wa gazeti moja la vijana, alisema kwamba kubalehe ni kama “kutembea juu ya kamba iliyoning’inizwa hewani bila kitu cha kukukinga unapoanguka chini.” Kwa kweli, kipindi hicho kigumu maishani kinaweza kumfanya mtu akose uhakika, awe na wasiwasi mwingi, na kuvurugika sana. Weill anaandika: “Vijana wanaobalehe hukabili magumu ya utoto na utu uzima.”

Ikiwa wewe ni kijana anayebalehe, utakabilianaje na magumu hayo? Ikiwa wewe ni mzazi wa kijana anayebalehe, ni nini kinachoweza kukusaidia kukumbuka jinsi miaka hiyo migumu ilivyokuwa ili uelewe vizuri yale ambayo mwana au binti yako anakabili? Katika mfululizo huu, tunawaomba vijana na watu wazima kuchunguza kwa makini kipindi cha kubalehe. Kufanya hivyo kutawasaidia vijana kuvumilia na hata kufanikiwa.