Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Kinanisaidia Kuvumilia Majaribu’

‘Kinanisaidia Kuvumilia Majaribu’

‘Kinanisaidia Kuvumilia Majaribu’

Hivyo ndivyo msomaji mmoja kutoka Connecticut, Marekani, alivyokifafanua kitabu Mkaribie Yehova. Alisema, “Ninajifunza sehemu ndogo ya kitabu hiki kila siku. Wakati ambapo nimeshuka moyo hivi kwamba ninashindwa hata kupumua, kujifunza kidogo kitabu hiki hunisaidia kuvumilia jaribu hilo.”

Anaendelea kusema: “Picha ya mchungaji mwenye huruma iliyo kwenye ukurasa wa 69 ilinichangamsha. Na nilithamini maelezo yaliyo kwenye ukurasa wa 28, fungu la 8, kuhusu kisa cha Musa kwenye kichaka kilichowaka moto ambayo yalisema kwamba ‘ardhi yote iliyokuwa karibu ikawa takatifu kwa sababu Yehova alikuwa akitumia sehemu hiyo!’ Ikiwa Yehova anaweza kufanya udongo uwe mtakatifu, basi mimi pia nina tumaini. Jambo hilo limenisaidia sana kwa sababu mimi hushuka moyo mara kwa mara.”

Tunaamini kwamba utafaidika kwa kusoma kitabu hiki chenye jalada nyepesi cha kurasa 320 chenye kichwa, Mkaribie Yehova. Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na uitume ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Mkaribie Yehova bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.