Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Ukulima Ninaandika kuwashukuru kwa mfululizo wa makala wenye kichwa “Kwa Nini Wakulima Wanakabili Matatizo?” (Oktoba 8, 2003) Ninaishi katika eneo lenye wakulima wengi. Kwa sababu ya hali mbaya za kiuchumi na matatizo mengine, wakulima wanauza mashamba yao. Ni kana kwamba kila siku nyumba zinajengwa mahali palipokuwa na mashamba. Wakati mwingine mimi hujiuliza ikiwa mashamba yatabaki kwa ajili ya ukulima. Inafariji kujua kwamba Yehova atasuluhisha kabisa matatizo ya wakulima.

V. A., Marekani

Picha za Mawe Asanteni kwa makala yenye kichwa “Picha Zilizotengenezwa kwa Mawe.” (Oktoba 8, 2003) Katika makala hiyo kulikuwa na picha ya mawe inayopatikana katika bustani moja ya umma katika eneo letu. Nimeishi karibu na bustani hiyo kwa zaidi ya miaka kumi, lakini sijawahi kuona picha hizo. Kwa hiyo nilienda kuziona na nilivutiwa sana. Sasa ninathamini sana picha zilizotengenezwa kwa mawe.

E. D., Marekani

Sikuzote nimetamani kujifunza zaidi kuhusu picha zilizotengenezwa kwa mawe, hasa tangu tulipohudhuria kusanyiko la Mashahidi wa Yehova huko Urusi mwaka wa 1993. Huko St. Petersburg na Moscow, tuliona picha nyingi maridadi za mawe. Tunawashukuru sana wasanii waliotumia miaka mingi kuzitengeneza na tunawashukuru ninyi kwa makala hiyo yenye kuarifu.

B. Z., Ujerumani

Ngono Isiyo ya Asili Asanteni kwa makala “Maoni ya Biblia: Je, Mungu Anakubali Ngono Isiyo ya Asili?” (Oktoba 8, 2003) Nina umri wa miaka 17 na nililelewa nikiwa Mkristo. Hata hivyo, nilianza kuwa na tamaa ya kufanya ngono na mtu wa jinsia yangu nilipokuwa mchanga sana. Imekuwa vigumu sana kuelewa tamaa yangu, lakini inafariji kwamba Yehova anaelewa pambano ninalokabili. Ningewatia moyo wote wanaopambana na hisia hizo wasikate tamaa!

J. M., Marekani

Katika maisha yangu yote nimeumia sana kihisia kwa sababu ya kuwa na tamaa zisizofaa za ngono. Makala yenu ilizungumzia hali yangu. Kutazama ponografia nikiwa mchanga sana na kutendewa vibaya kingono kumeniathiri sana. Asanteni kwa kunisaidia nijielewe.

J.B.M., Marekani

Tunapozungumzia mapendezi ya kingono, ni jambo la hekima kutaja kwamba mtu anaweza kuathiriwa na chembe za urithi, homoni, malezi, na mambo mengine mengi. Ni kweli kwamba mtu anayepambana na tamaa ya kufanya ngono na mtu wa jinsia yake anaweza kupata msaada katika kutaniko la Kikristo.

D. L., Uingereza

“Amkeni!” linajibu: Tunawahurumia sana wale wanaopambana na hisia za ngono. Kama vile makala yetu ilivyoonyesha, matatizo hayo yanaweza kusababishwa na mambo mengi mno. Lakini maadamu mtu hasitawishi tamaa mbaya au kutenda kupatana nayo kimakusudi, anaweza kuwa safi mbele za Yehova. Uwe na hakika kwamba Yehova Mungu hufurahi watu wanapofanya jitihada kama hizo za kudumisha usafi wa maadili.—Methali 27:11.

Vinu vya Upepo Nilifurahia makala “Vinu vya Upepo Vyatukumbusha Zama za Kale.” (Oktoba 8, 2003) Nilijifunza kwamba vinu vya upepo havikutumiwa tu kusaga nafaka bali pia vilikuwa na matumizi mengine mengi. Mimi ni mvulana wa mashambani, nami nashukuru sana kwa habari zote mnazochapisha.

S. A., Urusi

Athamini Amkeni! Asanteni kwa toleo la Oktoba 8, 2003. Ilikuwa mara yangu ya kwanza kusoma gazeti hilo kuanzia mwanzo hadi mwisho. Lakini nilianza kutambua kwamba ninapaswa kujifunza mambo yote ambayo Yehova anaandaa. Nilishangaa jinsi lilivyokuwa lenye kupendeza! Nimekuwa nikikosa mambo muhimu kwa kutosoma gazeti hilo zuri kuanzia mwanzo mpaka mwisho!

R. K., Japani