Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kilinipendeza Sana”

“Kilinipendeza Sana”

“Kilinipendeza Sana”

Hivyo ndivyo msomaji mmoja anayeitwa Lenita alivyoeleza kuhusu kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! Katika barua yake ya shukrani, Lenita alisema: “Lo! Kilinipendeza sana. Kitabu hicho kinaanza kama kitabu cha historia, na nilipoendelea kukisoma, nilihisi kana kwamba nilikuwa nikiishi katika siku za Danieli. Sikuwahi kamwe kukielewa kitabu cha Danieli jinsi hiyo.”

Aliongeza hivi: “Isitoshe, ni kitabu kizuri sana cha historia kwani kinaeleza kuhusu serikali kubwa za ulimwengu, mapambano, na watu waliohusika. Binti yetu mdogo ameanza kukisoma, nami ninapanga kumtia moyo akimalize na kukitumia kujifunza historia.”

Ikiwa ungependa kupokea kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! tafadhali jaza sehemu iliyo hapa chini na uitume ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.