Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Msamaria Mwema wa Leo

Msamaria Mwema wa Leo

Msamaria Mwema wa Leo

NA MWANDISHI WA AMKENI! NCHINI MEXICO

Wengi wetu tumesikia hadithi ya Biblia kuhusu mtu mwenye ujirani ambaye mara nyingi huitwa Msamaria Mwema. (Luka 10:29-37) Katika mfano huo, Yesu Kristo alionyesha jinsi Msamaria mmoja alivyojitahidi sana kuonyesha upendo kwa jirani yake mwenye uhitaji. Je, leo kuna watu walio kama huyo Msamaria mwema? Fikiria mfano unaofuata kutoka Mexico.

Betuel na familia yake walipokuwa wakirudi nyumbani kutoka safarini, waliona msiba mbaya sana wa barabarani kilometa chache kutoka kwao. Walisimama ili kusaidia. Mmoja wa madereva waliohusika ambaye ni daktari aliwaomba wampeleke mke wake mjamzito na binti zake wawili wadogo kwenye hospitali ya karibu ili watibiwe. Walifanya hivyo, na baadaye Betuel alirudi kwenye eneo la msiba ili kutoa msaada zaidi.

Betuel anasema: “Polisi wa barabarani walikuwa wamewasili, na daktari huyo alizuiliwa kwa ajili ya uchunguzi kwa sababu mtu fulani alikuwa amekufa. Daktari huyo aliponiuliza kwa nini ninamsaidia, nilimweleza kwamba sisi ni Mashahidi wa Yehova na tumejifunza katika Biblia kwamba tunapaswa kumpenda jirani yetu. Nilimwambia asiwahangaikie mke na watoto wake kwa kuwa tutawatunza. Alitokwa machozi na kushukuru kisha akanipa vitu vyake vyenye thamani ili nimtunzie.”

Betuel na familia yake walikaribisha familia ya mtu huyo nyumbani kwao na kuwatunza kwa siku kadhaa. Betuel alitumia nafasi hiyo kuanza kuwafundisha Biblia. Daktari huyo alipoachiliwa kutoka korokoroni, alitoa shukrani na kueleza jinsi alivyovutiwa na Mashahidi wa Yehova. Aliahidi kuendelea kujifunza Biblia katika mji wa kwao na kusema kwamba mke wake akijifungua mwana watamwita Betuel. Betuel anaendelea kusema: “Tuliwatembelea miaka miwili baadaye. Nilishangaa kujua kwamba wanaendelea kujifunza Biblia na kwamba mvulana wao mdogo anaitwa Betuel!”

[Picha katika ukurasa wa 13]

Betuel