Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Mafuta Ninawashukuru kwa mfululizo wa makala, “Mafuta—Je, Yatakwisha?” katika toleo la Novemba 8, 2003. Sijawahi kuona takwimu nyingine zenye kushangaza kama zile zilizoonyeshwa kuhusu umwagaji wa mafuta. Haishangazi kwamba dunia imeharibiwa na mwanadamu! Hilo hunifanya nitazamie wakati ambapo Yehova ataisafisha dunia na kuifanya kuwa paradiso milele!

T. T., Marekani

Makala hizo ziliandikwa kwa njia ya kupendeza na bila upendeleo. Ingawa nina shahada fulani ya fizikia sijawahi kusikia kwamba mafuta hayakutokana na viumbe. Kwa kawaida watu hufundishwa kwamba mafuta hutokea viumbe vinapooza.

E. B., Ufaransa

Niko katika chuo cha ufundi na imekuwa vigumu kwangu kupata vitabu vyenye chati za kuonyesha jinsi mashine zinavyofanya kazi. Hiyo ndiyo sababu nilipendezwa sana na ile chati inayoonyesha jinsi mafuta yanavyozalishwa. Ilifanya makala hiyo ieleweke kwa urahisi.

M. I., Japani

Mfululizo wenu ulipaswa kufanyiwa utafiti zaidi. Hamkutaja kwamba kisima cha kwanza cha kibiashara cha mafuta huko Amerika Kaskazini kilichimbwa na James Miller Williams huko Ontario, Kanada, mwaka mmoja kabla ya Edwin Drake kuchimba kisima cha Titusville, Pennsylvania, Marekani.

G. Y., Kanada

“Amkeni!” linajibu: Kuna ubishi mwingi kuhusu jambo hilo. Mwanajiolojia mmoja wa petroli ambaye ameandika kuhusu historia ya mafuta aliliambia “Amkeni!” kwamba “haijulikani waziwazi” mahali ambapo kisima cha kwanza cha mafuta kilichimbwa. Hivyo kitabu “The Canadian Encyclopedia” kinakata kauli hii: “Inadaiwa kwamba Williams na vilevile E. L. Drake wa Pennsylvania ndio waliokuwa wa kwanza kuchimba kisima cha kwanza cha mafuta katika Amerika Kaskazini.”

Jiografia Familia yetu inapenda makala zinazozungumzia jiografia. Hivyo tulifurahia ile makala “Mto Mkubwa wa Amazon Unawategemeza Mamilioni.” (Novemba 8, 2003) Ingawa tulijifunza kuhusu Mto Amazon shuleni, hatukutambua kwamba “kwa sekunde 30 tu, mto huo unaweza kuzima kiu cha wanadamu wote kwa siku moja”! Tunafurahi kwamba makala kama hizo hutuwezesha “kutembelea” maeneo ya mbali.

V. G., Slovakia

Asanteni sana kwa makala yenye kupendeza yenye kichwa “Prague—Jiji Lenye Historia ya Kuvutia.” (Novemba 8, 2003) Nilifurahia sana kusoma kuhusu jiji hilo la kihistoria—ni kana kwamba nilikuwa huko! Asanteni pia kwa picha maridadi.

L. Z., Urusi

Tukiwa shuleni tuliambiwa tuandike insha kuhusu jiji fulani na kulifafanua kwa njia ambayo ingefanya mtu atamani kulitembelea. Insha yangu ilitegemea makala kuhusu Prague, na nilipata maksi za juu zaidi darasani. Asanteni!

O. C., Ufaransa

Watu wa Ukoo Ambao Si Waamini Asanteni kwa makala “Maoni ya Biblia: Ufanye Nini Iwapo Watu wa Ukoo Si wa Dini Yako?” (Novemba 8, 2003) Kwa kuwa mimi ndiye Mkristo pekee katika familia yetu ya watoto sita, nimejitahidi kwa miaka mingi kushughulikia hali hiyo kwa busara. Nilijifunza mengi kutokana na maandiko yaliyoonyeshwa katika makala hiyo!

R. G., Marekani

Nilianza kujifunza Biblia karibuni. Lakini mimi hujitahidi kuwaambia watu wangu wa ukoo, ambao si waamini, mambo machache ninayoyajua. Kwa sababu nina umri wa miaka 16 tu, familia yetu haijaniruhusu kubatizwa, lakini ninatumaini nitabatizwa siku moja. Makala hiyo itanisaidia kushughulika na familia yetu.

J. G., Marekani