Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Utasoma Habari Zote Hizi Lini?”

“Utasoma Habari Zote Hizi Lini?”

“Utasoma Habari Zote Hizi Lini?”

Katika Julai 2001, mtu mmoja huko Khabarovsk, mashariki mwa Urusi, alipata rundo la magazeti 34 ya Amkeni! katika maktaba ya jiji. Mtu huyo aliazima magazeti hayo lakini wakati wa kuyarudisha ulipofika katika mwezi wa Agosti hakutaka kufanya hivyo. Kwa hiyo akayaazima tena hadi mwezi wa Septemba. Alipenda magazeti hayo sana, naye akayaazima tena mwezi wa Novemba, kutia ndani matoleo sita mapya ya Amkeni!

Kabla ya tukio hilo mtu huyo aliepuka kusoma vichapo vya kidini. Basi, kwa nini alianza kusoma magazeti ya Amkeni!? Yeye anaandika: “Ni kwa sababu makala nyingi za gazeti hili huzungumzia matatizo ya kijamii, ambayo huwahangaisha watu wote.”

Aliongeza hivi: “Mara nyingi, kuna makala zilizoandikwa vizuri kuhusu majiji na nchi nyingi za leo, kutia ndani habari kuhusu tamaduni za watu mbalimbali.” Mtu huyo pia alivutiwa na makala kuhusu watu waliofanikiwa maishani, wakadumisha hali yao ya kiroho, na kuwasaidia wengine kuvumilia magumu na misiba. Alilinganisha magazeti hayo na nini? “Bila shaka inaweza kusemwa kwamba gazeti la Amkeni! ni kama magazeti Time, Popular Science, na National Geographic yakiwekwa pamoja!”

Mtu huyo aliomba apelekewe matoleo ya miaka iliyopita ya Amkeni! katika Kirusi kuanzia matoleo ya mwaka wa 1995. Zaidi ya hilo, aliomba vitabu mbalimbali na broshua zinazochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Yeye anaandika hivi: “Huenda ukaniuliza, ‘Utasoma habari zote hizi lini?’” Kisha akajibu swali lake mwenyewe kwa kusema kwamba ana wakati wa kusoma habari zinazofaa, kwani hatumii muda mwingi akitazama televisheni au akitumia kompyuta.

Amkeni! hueleza mengi kuhusu matukio ya karibuni na jinsi ya kusuluhisha matatizo ya leo. Kwa nini usiwaulize Mashahidi wa Yehova wakuletee matoleo mapya ya Amkeni! kila mwezi?

[Picha katika ukurasa wa 31]

Watoto Wanahitaji Nini Kutoka kwa Wazazi?

[Picha katika ukurasa wa 31]

Kuyaelewa Magonjwa ya Kihisia

[Picha katika ukurasa wa 31]

Je, Unajua Jina la Mungu?

[Picha katika ukurasa wa 31]

Je, Kweli Kuna Tisho la Nyuklia?

[Picha katika ukurasa wa 31]

Unaweza Kupata Wapi Tumaini?

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 31]

Nuclear explosion: U.S. Department of Energy photograph