Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kodi Nimekuwa nikifanya uchunguzi kuhusu kodi kwa majuma kadhaa yaliyopita. Nilijiuliza maswali mbalimbali, kwa mfano, Kutoza kodi kulianza lini? Nilipokuwa nikiendelea na uchunguzi wangu, mke wangu alipewa toleo la Amkeni! la Desemba 8, 2003, lililokuwa na mfululizo wenye kichwa “Je, Unalipa Kodi Nyingi Sana?” Nilifurahi sana nilipojua kwamba makala hizo zinazungumzia masuala niliyokuwa nikichunguza.

S. Y., Tajikistan

Kutiwa Damu Mishipani Mimi ni daktari na pia mhubiri wa wakati wote. Ninawashukuru sana kwa kuchapisha simulizi la Yasushi Aizawa, lenye kichwa, “Nilikubali Maoni ya Mungu Kuhusu Damu.” (Desemba 8, 2003) Hali yake ilifanana sana na yangu, kwani nilihitaji kujifunza kutotanguliza kazi yangu ya udaktari maishani mwangu. Yaelekea nitakutana na Ndugu Aizawa katika ulimwengu mpya wa Mungu, ambapo hatutakuwa madaktari. Wakati huo madaktari hawatahitajiwa hata kidogo!

A. S., Ekuado

Katika Oktoba 2002, iligunduliwa kwamba binti yetu mdogo anaugua ugonjwa wa kansa. Matibabu yake yalihusisha mambo mengi, kwani yalitia ndani kupasuliwa mara mbili, matibabu ya kemikali, na matibabu mengine ya pekee. Wakati wote huo, tulijitahidi sana kutii amri ya Biblia ya kujiepusha na damu. Hilo lilikuwa jambo gumu, kwani karibu watoto wote wanaotibiwa kwa kemikali nchini Lithuania hutiwa damu mishipani. Makala yenye kichwa, “Nilikubali Maoni ya Mungu Kuhusu Damu,” ilituimarisha kutii amri hiyo ya Yehova. Sasa binti yetu anapata nafuu.

M. na S. D., Lithuania

Mashindano Kati ya Ndugu Ninawashukuru sana kwa makala “Vijana Huuliza . . . Nawezaje Kujijengea Jina Bila Kuwategemea Ndugu Zangu?” (Novemba 22, 2003) Nina miaka 16, nami huona kwamba dada yangu mkubwa ndiye anayetambuliwa nyakati zote. Ninajua kwamba Yehova ananijali, hata hivyo, ninahisi upweke. Makala hiyo ilishughulikia tatizo langu. Kwa kuwa makala hiyo iliandikwa kwa fadhili sana, nililia nilipoisoma. Asanteni kwa mashauri hayo mazuri. Yalinisaidia kuwa na maoni yanayofaa.

M. O., Japani

Mara kwa mara mimi huhisi kama vijana wote waliotajwa katika makala hiyo. Nyakati zote dada yangu mkubwa ameonwa kuwa mfano mzuri. Hivyo, ninajua jinsi mtu anavyohisi anapolinganishwa kila mara na mshiriki mwingine wa familia. Maelezo katika makala hiyo yaliyoonyesha kwamba mtu anapaswa kutambua vipawa vyake, yalikuwa kama “matunda ya mtofaa ya dhahabu kwenye chombo cha fedha kilichopambwa,” yaani yalikuwa maneno yaliyosemwa wakati unaofaa.—Methali 25:11.

S. T., Marekani

Nina dada mkubwa na ndugu mdogo. Wao hufanikiwa sana kufanya mambo kuliko mimi. Kwa hiyo, nilifuata mashauri yenu nami sasa najifunza Kihispania na pia ninahubiri kwa ukawaida. Ninafurahia kujifunza, na watu wanapendezwa nami.

H. B., Marekani

Ni Nini Kitakachoupata Ulimwengu? Katika makala yenye kichwa “Dini Yangu Ilikuwa Sayansi” (Septemba 22, 2003), inaonekana kwamba Kenneth Tanaka hajui kuwa wanasayansi wanaamini ulimwengu utaendelea kupanuka milele.

R. G., Marekani

“Amkeni!” linajibu: Maoni ya wataalamu wa anga hayapatani. Kwa mfano, baadhi yao husema kwamba mwendo wa kupanuka kwa ulimwengu utapungua, kisha ulimwengu utaacha kupanuka na kuanza kusongamana na hatimaye kuangamia. Maelezo ya Kenneth Tanaka yaligusia nadharia zote mbili, hata hivyo, hakuziunga mkono kwa vyovyote. Alitoa maelezo hayo ili kuonyesha jitihada yake ya kutafuta kusudi la maisha, na kwamba sayansi haiwezi kueleza mambo yote.