Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Wajua?

Je, Wajua?

Je, Wajua?

(Majibu ya maswali haya yanapatikana katika maandiko ya Biblia ambayo yameonyeshwa, na orodha kamili ya majibu imechapwa katika ukurasa wa 26. Unaweza kupata habari zaidi katika kichapo “Insight on the Scriptures,” kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.)

1. Ili kukazia kwamba hatupaswi ‘kurudia vitu vilivyo nyuma,’ Yesu Kristo hutuhimiza tumkumbuke nani? (Luka 17:31, 32)

2. Katika mfano wa Yesu wa mpandaji, kwa nini mbegu iliyochipuka kwenye udongo wenye miamba ilinyauka? (Marko 4:5, 6)

3. Inamaanisha nini kwamba Yesu aliyefufuliwa angeketi kwenye ‘mkono wa kuume’ wa Yehova? (Matendo 2:34)

4. Ni Mshua yupi mmoja anayetajwa katika Maandiko? (Ayubu 8:1)

5. Mungu alimpa Yakobo jina gani alipokuwa na umri wa miaka 97 hivi? (Mwanzo 32:28)

6. Ingawa Sauli hakumtii Mungu na alikuwa akimkimbiza Daudi, kwa nini Daudi hakumuua Sauli wakati alipopata nafasi ya kufanya hivyo? (1 Samweli 26:7-11)

7. Kwa utimizo wa maneno ya Yehova, ni wanyama gani waliomla Yezebeli? (2 Wafalme 9:36)

8. Waisraeli walipokuwa wakielekea kwenye Bahari Nyekundu, kituo chao cha kwanza kinachotajwa katika Biblia kilikuwa wapi? (Kutoka 12:37)

9. Kama Yakobo alivyosema, ni ibada ipi iliyo “safi na isiyotiwa unajisi kwa maoni ya Mungu wetu”? (Yakobo 1:27)

10. Ni kipindi gani cha wakati ambacho Danieli alijulishwa ili kuonyesha wakati ambapo Masihi angetokea na kukatiliwa mbali? (Danieli 9:24-27)

11. Yesu alisema ni nini ‘kingehubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote’ kabla ya mwisho? (Mathayo 24:14)

12. Yale “matendo ya mwili” yanayomzuia mtu kurithi Ufalme wa Mungu ni yapi? (Wagalatia 5:19-21)

13. Ni nini humwezesha Yehova kumhukumu mtu kwa usahihi? (1 Samweli 16:7)

14. Kabla ya kuchaguliwa kuwa nabii, Amosi alikuwa akifanya kazi gani? (Amosi 7:14)

15. Yesu alimaanisha nini aliposema kwamba wanafunzi wake wanapaswa ‘kuwachukia’ watu wa familia zao? (Luka 14:26)

Majibu ya Maswali

1. “Mke wa Loti”

2. Kwa sababu haikuwa na mzizi haingeweza kustahimili joto lenye kuunguza

3. Yesu angekuwa na cheo kikubwa zaidi, ambacho ni cha pili kutoka kwa Yehova mwenyewe

4. Bildadi, mmoja wa waandamani watatu wa Ayubu

5. Israeli

6. Kwa kuwa Sauli alikuwa ametiwa mafuta na Yehova, Daudi aliacha jambo hilo mikononi mwa Yehova

7. Mbwa

8. Sukothi

9. “Kuwatunza mayatima na wajane katika dhiki yao, na kuendelea kujitunza bila doa kutokana na ulimwengu”

10. “Majuma 70”

11. “Habari njema ya Ufalme”

12. “Uasherati, uchafu, mwenendo mpotovu, ibada ya sanamu, mazoea ya kuwasiliana na pepo, uadui, mizozo, wivu, milipuko ya hasira, magomvi, migawanyiko, madhehebu, husuda, vipindi vya kulewa, karamu za kupindukia, na mambo kama hayo”

13. Yeye “huona jinsi moyo ulivyo”

14. Alikuwa “mchungaji na mminyaji wa tini za mikuyu”

15. Kwamba wanapaswa kuwapenda watu wa familia zao kwa kadiri ndogo kuliko vile wanavyompenda Yesu