Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kitu Ambacho Vijana Wanahitaji

Kitu Ambacho Vijana Wanahitaji

Kitu Ambacho Vijana Wanahitaji

Kwa miaka kadhaa sasa wazee na vijana ambao wamesoma kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, wamesema kwamba kitabu hicho huwapa vijana habari wanazohitaji hasa. Msichana mmoja katika jimbo la Sinaloa, huko Mexico, aliomba nakala kumi za kitabu hicho kwa ajili ya marafiki zake. Alisema kwamba ijapokuwa yeye si Shahidi wa Yehova, anakipenda sana kitabu hicho, kisha akaongeza hivi: “Ninawaheshimu sana.”

Alisema hivi: “Mimi nina marafiki wengi ambao wana maswali mengi kuhusu maisha yao ya sasa. Nimewaonyesha kitabu hicho, nacho kimewapendeza sana. Kitabu hicho ni kizuri wee! Kina habari zote ambazo kijana anahitaji.” Aliomba kupata vitabu alivyoagiza kabla ya kwenda likizo.

Kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza kina sura 39. Baadhi ya sura hizo ni: “Niwafanyeje Wazazi Wangu Wanipe Uhuru Zaidi?” “Naweza Kufanyaje Marafiki wa Kweli?” “Vipi Juu ya Ngono Kabla ya Ndoa?” na “Nijueje Kama Ni Upendo Halisi?” Unaweza kuomba kitabu hicho chenye kurasa 320 kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa hapa chini au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.