Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Watoto Mara tu nilipopokea mfululizo wenye kichwa “Watoto Wanahitaji Nini Kutoka kwa Wazazi?” niliusoma kwa hamu. (Desemba 22, 2003) Nilipendezwa sana na makala hizo kwani mimi ni mama ya watoto watano. Ningependa kila mama asome makala hizo.

C. M., Ufaransa

Makala mnazochapisha ni za wakati unaofaa. Mimi na mume wangu tulipojua kwamba tutapata mtoto, mlichapisha makala kuhusu wanawake wajawazito. (Januari 8, 2003) Sasa tukiwa wazazi wenye furaha wa mtoto aliye na umri wa miezi mitatu, mmechapisha makala zenye madokezo mazuri kuhusu kumlea mtoto mchanga. Makala hizo zinaweza kumsaidia sana mwanamke kijana aliyepata mtoto karibuni.

D. K., Poland

Simulizi la Maisha Asanteni sana kwa makala zote mnazochapisha. Hata hivyo, mimi hupenda hasa makala za masimulizi ya maisha. Lile simulizi la Eileen Brumbaugh lenye kichwa, “Mavazi na Mapambo Yalinizuia Kufanya Maendeleo,” lilinigusa moyo. (Desemba 22, 2003) Ama kweli, alitamani sana kuipata dini ya kweli!

L. M., Urusi

Nilipendezwa hasa na simulizi la Eileen Brumbaugh kwa sababu katika eneo letu kuna familia nyingi zinazoshirikiana na dini ya Amish na Mennonite. Mwanzoni sikuona faida ya kuwahubiria kwani inaonekana kwamba wameshikilia sana imani yao. Kisa chake kimenisaidia kutambua kwamba tukipendezwa kibinafsi na kuwahangaikia watu wa namna zote, tunaweza kuwasaidia kupata ujuzi sahihi juu ya Mungu.

M. H., Marekani

Nimekuwa nikifikiri kwamba vipodozi na vito vinapaswa kutumiwa tu na “walimwengu.” Upendo usio na unafiki ambao Mashahidi wa Yehova huonyesha pamoja na staha yao kwa Biblia, zimenifanya niache kutazama sura ya nje tu.

A. C., Marekani

Mitishamba Nilifurahia kusoma makala yenye kichwa “Je, Mitishamba Inaweza Kukusaidia?” (Desemba 22, 2003) Mimi ni muuguzi aliyesajiliwa, nami hutumia aina mbalimbali za mitishamba kutuliza maumivu ya viungo vyangu. Mitishamba imenisaidia sana. Hata hivyo, hamkutaja kwamba baadhi ya mitishamba humfanya mtu atokwe damu sana wakati wa upasuaji. Mashahidi wa Yehova wanapaswa kufikiria kwa uzito uhitaji wa kuacha kutumia mitishamba fulani kabla ya kufanyiwa upasuaji.

J. H., Marekani

“Amkeni!” linajibu: Asante sana kwa kutukumbusha jambo hilo muhimu. Kabla ya upasuaji, mgonjwa anapaswa kumweleza daktari kuhusu dawa zozote ambazo anatumia, kutia ndani mitishamba. Hilo ni muhimu sana kwa wale ambao hutii sheria ya Biblia ya ‘kujiepusha na damu.’—Matendo 15:29.

Kusema Mbele ya Watu Nilifurahia sana kusoma ile makala “Vijana Huuliza . . . Nawezaje Kufaulu Kusema Mbele ya Watu?” (Desemba 22, 2003) Nimekuwa mwandishi wa habari kwa miaka kumi, hata hivyo, mimi huwa na wasiwasi kila mara ninaposema mbele ya watu wengi. Maagizo mazuri ambayo nimepokea kupitia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, inayofanywa katika Majumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova, ni bora kuliko yale niliyopata shuleni na kazini. Zaidi ya kunisaidia kuboresha ustadi wangu wa kuhubiri nyumba kwa nyumba, mazoezi hayo yamenisaidia kufanikiwa kazini.

L. B., Marekani