Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Jina la Mungu Tangu niwe Mkristo mwaka wa 1973, sijasoma makala inayofafanua vizuri sana habari kuhusu jina la Mungu kama ule mfululizo wenye kichwa “Je, Unajua Jina la Mungu?” (Januari 22, 2004) Picha inayovutia kwenye jalada la gazeti hilo na zile sababu zenye nguvu zilizotolewa kwa utaratibu, hufanya makala hiyo iwe ya pekee. Hongera!

D. L., Marekani

Hivi karibuni nilianza kutumikia nikiwa mhubiri wa wakati wote, nami nahisi nimemkaribia Yehova zaidi. Hilo lilifanya nipendezwe sana na ule mfululizo kuhusu jina la Mungu. Lile sanduku lenye kichwa “Mungu Anajua Jina Lako,” lilionyesha kwamba ijapokuwa kuna watu wengi duniani, Mungu anajali kila mmoja wetu. Jambo hilo limenifanya nitamani kujifunza mengi kumhusu Yehova na kufanya mapenzi yake.

M. J., Japani

Nilipokuwa nikisoma mfululizo huo nilitambua kwamba ni wenye kuarifu, unashughulikia suala hilo kwa urefu, na kwamba umefanyiwa utafiti mwingi na kuandikwa kwa njia yenye kupendeza na kuvutia sana. Pia nilifurahia kuona jina la Mungu katika lugha 39, likiwa limeandikwa juu ya kurasa za gazeti hilo. Makala hizo hutukuza jina la Yehova, nazo huwapendeza watu wanyofu.

G. D. M., Marekani

Imani ya Mwanasayansi Nilipendezwa sana na Makala yenye kichwa “Kwa Nini Naamini Biblia?—Mwanasayansi wa Nyuklia Aeleza.” (Januari 22, 2004) Miaka sita iliyopita, mimi pia nilisadikishwa kuhusu ukweli wa Biblia kwa kutegemea sababu zilizotolewa kwa utaratibu na vilevile mambo yaliyothibitishwa. Sasa mimi nayapenda sana yale niliyojifunza. Simulizi kama lile la Alton Williams, yameimarisha imani yangu. Ninamshukuru Yehova kwa kumpa kila mmoja wetu uthibitisho unaomfaa yeye binafsi.

E. L., Hungaria

Maua ya Afrika Ninawaandikia ili kuwashukuru kwa sababu ya makala yenye kichwa “Muujiza wa Kila Mwaka wa Namaqualand.” (Januari 22, 2004) Inastaajabisha sana kuona maua ya aina nyingi tofauti-tofauti ambayo Yehova ameumba ili tuyafurahie. Nilipokuwa nikisoma makala hizo, nilikumbuka maneno haya ya mtunga-zaburi Daudi: “Kazi zako ni za ajabu, kama vile nafsi yangu inavyojua vema.”—Zaburi 139:14.

A. J., Mexico

Kazi ya Shule Niko katika kidato cha kwanza, na mara nyingi mimi hushindwa kuratibu wakati wangu. Kusoma makala “Vijana Huuliza . . . Nawezaje Kupata Wakati wa Kufanya Kazi za Shule?” kulinisaidia sana. (Januari 22, 2004) Sikuwa nikitazama televisheni sana. Lakini nilipoitazama, ningetazama kipindi kimoja baada ya kingine. Sasa siitazami hata kidogo.

R. O., Japani

Ninasomea nyumbani, na ni wazi kwamba mtu anapaswa kujitahidi sana ili ajifunze kila siku. Nikifuata madokezo mliyotoa nitapata nafasi ya kufanya kazi zangu za shule.

X. R., Marekani

Ninakubali kwamba kazi za shule hunilemea. Nyakati nyingine ninapotumia muda mrefu kuzifanya, wazazi wangu hufikiri kwamba mimi ni mvivu. Hata hivyo, nyakati nyingine kazi hizo huwa ngumu sana nazo huwa nyingi. Asanteni sana kwa kutuonyesha jinsi tunavyoweza kupata wakati wa kufanya kazi hizo na kutumia wakati wetu vizuri.

J. S., Marekani

Makala hiyo ilinisaidia sana. Madokezo chini ya kichwa “Kutumia Wakati Vizuri,” yalinisaidia kuboresha mazoea yangu ya kujifunza.

B. L., Italia