Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Zinaweza Kuwafariji Wale Wanaoomboleza

Zinaweza Kuwafariji Wale Wanaoomboleza

Zinaweza Kuwafariji Wale Wanaoomboleza

Mwanamke mmoja huko Jalisco, Mexico, aliandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova hivi: “Tafadhali nitumieni nakala kadhaa za broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Mimi si Shahidi wa Yehova, hata hivyo, ninaamini mambo mengi mnayofundisha.”

Alisema hivi kuhusu kusudi la kuandika barua hiyo: “Nataka broshua hizo kwa sababu ninajua kwamba zitawafariji wateja kwenye duka letu la maua. Ninazungumza hasa kuhusu wateja ambao huja kununua maua ili kuyaweka kwenye makaburi, na ambao mara nyingine huwa wamefiwa na mke, mume, au mzazi. Ninahisi kwamba broshua hizo zitawasaidia sana.”

Huenda wewe au mtu fulani unayemjua akafarijiwa kwa kusoma broshua hiyo yenye kurasa 32. Inajibu maswali kama vile: Ninaweza kuishije nikiwa na huzuni yangu? Wengine wanaweza kusaidiaje? Wafu wana tumaini gani?

Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.