Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Kuishi Pamoja Bila Kuoana Ni Msingi Mzuri wa Ndoa?

Je, Kuishi Pamoja Bila Kuoana Ni Msingi Mzuri wa Ndoa?

Je, Kuishi Pamoja Bila Kuoana Ni Msingi Mzuri wa Ndoa?

JARIDA Journal of Marriage and Family linasema kwamba visa vya mwanamume na mwanamke kuishi pamoja bila kufunga ndoa, “vimekuwa vya kawaida katika nchi zilizoendelea ulimwenguni pote.” Pia jarida hilo linasema kwamba “asilimia 50 hivi ya watu wanaoishi pamoja bila kufunga ndoa huona hiyo kuwa njia bora ya kuchunguza ikiwa wanafaana kabla ya kuingia katika kifungo cha ndoa.” Ikiwa maoni hayo ni sahihi, jarida hilo linasema kwamba ingetazamiwa “jambo hilo litatue kabisa matatizo ya kutofaana katika ndoa.”

“Hata hivyo, uthibitisho unapingana na maoni hayo,” lasema jarida hilo. Kisha linaongezea: “Wenzi wanaoishi pamoja kabla ya kufunga ndoa, hawaridhiki na maisha ya ndoa, hutumia wakati mfupi pamoja na wenzi wao wa ndoa, hukosana mara nyingi, hawategemezani sana, mara nyingi hawafanikiwi kusuluhisha matatizo, nao huwa na matatizo mengi ya ndoa . . . Isitoshe, wao hutalikiana kwa urahisi, wakilinganishwa na wale ambao hufunga ndoa kabla ya kuanza kuishi pamoja.”

Uchunguzi huo unaonyesha kwamba mwendo unaodhaniwa kuwa wa hekima machoni pa mwanadamu huenda ukawa wa kipumbavu. Jambo hilo huonyesha ukweli wa maneno haya yanayopatikana katika Yeremia 10:23: “Mwanadamu . . . hana uwezo wa kuongoza hatua yake.” Je, si jambo la hekima zaidi kufuata mashauri bora kuhusu ndoa yanayopatikana katika Neno la Mungu Biblia? (2 Timotheo 3:16) Kwa mfano, Biblia husema hivi kuhusu ndoa: “Mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake nao watakuwa mwili mmoja.”—Mwanzo 2:24; Mathayo 19:5.

Kutii mwongozo huo kutoka kwa Mungu, badala ya kufuata maoni ya mwanadamu yanayobadilika-badilika, kutachangia kwa kadiri kubwa uwezekano wa kuwa na ndoa itakayodumu na iliyo na furaha.—Methali 3:5, 6.