Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Msaada wa Kutatua Matatizo ya Familia

Msaada wa Kutatua Matatizo ya Familia

Msaada wa Kutatua Matatizo ya Familia

Mwanamke mmoja kutoka Veracruz, Mexico, alipewa gazeti la Amkeni! lililozungumzia tatizo lililokuwa katika familia yake. Aliandika hivi: “Gazeti hilo lilinipendeza sana kwa sababu habari zenyewe zilinihusu.” Barua aliyoandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ilisema hivi pia: “Habari hii itanisaidia mimi, mume wangu, na watoto wetu.”

Mwanamke huyo aliongeza hivi: “Ningependa kujua mengi zaidi kuhusu Mashahidi wa Yehova na kutaniko lililo karibu na mahali ambapo ninaishi. Ningependa kuhudhuria mikutano yenu pamoja na familia yangu kwa sababu ninaona kwamba tunahitaji kumkaribia Mungu zaidi.” Kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia kilikuwa kimeonyeshwa katika ukurasa wa mwisho wa gazeti la Amkeni! ambalo lilikuwa limemvutia mwanamke huyo. Kwa hiyo akaomba nakala moja.

Kitabu hicho kinazungumzia mambo yanayohusu kila mtu katika familia, awe ni mume, mke, mzazi, mtoto, babu, au nyanya. Baadhi ya sura zake zilizo na masomo muhimu ni, “Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana,” “Saidia Tineja Wako Asitawi,” “Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu,” na “Dumisha Amani Nyumbani Mwako.”

Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.