Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kilimsaidia Mtoto Huyu

Kilimsaidia Mtoto Huyu

Kilimsaidia Mtoto Huyu

Miaka fulani iliyopita, Savinien, mvulana mwenye umri wa miaka tisa anayeishi katika mji mdogo huko Pennsylvania, Marekani, aliandika barua ili kushukuru kwa ajili ya kitabu chenye kichwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Kijana huyo alisema kwamba alikuwa amemaliza kusoma kitabu hicho ambacho kina picha nyingi za watu na matukio yaliyo katika Biblia.

Aliwaandikia hivi wachapishaji wa kitabu hicho: “Ninahisi kwamba mnapaswa kuendelea kuchapisha kitabu hiki ili mwendelee kuwatia moyo watoto wadogo kama mimi wafahamu mengi zaidi kuhusu Biblia.

“Nimejifunza katika kitabu hiki kwamba kila kitu kilichoandikwa katika Biblia ni cha kweli, na kwamba kiliandikwa ili kutufundisha na kutupatia tumaini la wakati ujao.

“Singejua mambo hayo ikiwa hamngependezwa na vijana na kurahisisha habari hii ili tuweze kuielewa vizuri zaidi.”

Umefanya nini ili kumsaidia mtoto wako ajifunze? Unaweza kuomba kitabu hicho cha kurasa 256 chenye kichwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, kilicho na hadithi 116 zinazohusu watu na matukio ya Biblia. Jaza sehemu iliyo hapa chini na uitume ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu chenye kichwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.