Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Maprofesa Wangu Walifurahi Sana”

“Maprofesa Wangu Walifurahi Sana”

“Maprofesa Wangu Walifurahi Sana”

Hivyo ndivyo mwanafunzi fulani katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Jimbo la Tbilisi nchini Georgia alivyosema alipowaandikia wachapishaji wa Amkeni! Kwa nini mwanafunzi huyu aliwaandikia?

“Nimekuwa nikisoma magazeti yenu tangu mwaka wa 1998. . . . Hayo hunisaidia sana katika masomo yangu. Makala hizo huchapishwa kwa wakati unaofaa nazo huwa na habari nyingi zinazotegemeka. Hivi majuzi nilitumia ule mfululizo wa makala katika Amkeni! la Novemba 22, 2002, uliokuwa na kichwa, ‘Je, Sayansi Imevuka Mipaka kwa Kutumia Chembe za Msingi?’ kuandika insha juu ya ‘Kufanyiza Kiumbe Pacha na Aina za Chembe za Msingi.’ Maprofesa wangu walifurahi sana, nami nilipata alama za juu zaidi.

“Ninafurahi sana kwamba nyinyi huchapisha makala kama hizo zenye kupendeza, hasa kuhusu tiba. Hata ingawa hakuna yeyote katika familia yetu aliye mmoja wa Mashahidi wa Yehova, sisi hufurahia sana magazeti yenu, kwani yanaongeza ujuzi wetu kuhusu ulimwengu unaotuzunguka.”

Huenda ukashangaa kujua kwamba Biblia ina mashauri ambayo mtu anaweza kutumia yanayochangia afya nzuri ya mwili na akili. Jambo hilo linakaziwa katika broshua inayovutia yenye kurasa 32 ambayo ina kichwa Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote. Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.