Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kitabu cha Vijana Kinachosifiwa Sana

Kitabu cha Vijana Kinachosifiwa Sana

Kitabu cha Vijana Kinachosifiwa Sana

MWALIMU mkuu wa Shule ya Wasichana ya Tigoni, katika mji wa Limuru nchini Kenya, aliiandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova akiomba nakala za kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Alisema hivi: “Kama mnavyojua, si rahisi kushughulika na vijana. Tuna nakala mbili za kitabu chenu, ambazo zimewasaidia walimu na wanafunzi. Kitabu hicho kina habari za kutosha na kinashughulikia mahitaji yetu na yale ya vijana wetu.”

Mwalimu huyo mkuu alisema: “Wasimamizi wa shule hii wangependa kitabu hicho kinachonufaisha kitumiwe kuwafundisha wanafunzi wetu. Wanakipenda. Wazazi wa shule hii wanaunga mkono jitihada zetu za kuwasaidia watoto wao. Tunafikiri kwamba kwa sasa nakala 25 za kitabu hicho zitatosha.”

Kitabu Vijana Huuliza huzungumzia mambo ambayo vijana huwaza na kuhisi. Kinachochea watu wazungumzie mambo mbalimbali yanayofaidi kama vile: “Niwafanyeje Wazazi Wangu Wanipe Uhuru Zaidi?,” “Je, Niondoke Nyumbani?,” “Naweza Kufanyaje Marafiki wa Kweli?,” “Nichague Kazi-Maisha Gani?,” “Vipi Juu ya Ngono Kabla ya Ndoa?,” na “Nijueje Kama Ni Upendo Halisi?”

Hivyo ni baadhi ya vichwa katika kitabu hicho. Katika sura zake 39, kitabu hicho kinazungumzia mambo mengine mengi. Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.