Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Tumaini Tunaandika barua hii fupi ili kuwashukuru kwa ajili ya mfululizo wenye kichwa “Unaweza Kupata Wapi Tumaini?” (Aprili 22, 2004) Tulisoma makala hiyo kama familia na tulipoimaliza tulikuwa karibu kutokwa na machozi. Picha ya ua ilivutia sana.

H. H. & L. H., Marekani

Mama yangu alikufa juma moja kabla sijapokea gazeti hilo, hivyo, nilifarijiwa sana na maneno haya: “Wafu wako katika hali salama kabisa, jinsi mtoto alivyo salama katika tumbo la uzazi la mama yake.” Bado naomboleza kifo cha mama yangu, lakini ninafurahi kwamba yuko katika kumbukumbu la Yehova.

V. L., Marekani

Nimekuwa nikisoma gazeti Amkeni! kwa miaka 50 hivi, nalo hunivutia kwa sababu kila mara nyinyi huandika kuhusu jambo ambalo mmezungumzia mara nyingi lakini mnaliandika kwa njia tofauti kabisa. Habari mliyoandika kuhusu kuwa na maoni mabaya ilifaa sana.

T. H., Marekani

Nina ugonjwa usioweza kupona. Mimi hujaribu kuwa na maoni yanayofaa, lakini leo niliamka nikiwa nimekata tamaa. Kwa hiyo nilisoma makala hizo tena na tena. Makala hizo zilizungumzia mambo yenye kufariji nami nilifarijiwa sana nazo.

B. J., Uingereza

Mume wangu anaugua kansa. Kuwatunza watoto wetu kulinifadhaisha sana. Pia, nimepoteza kazi. Lakini ile sehemu yenye kichwa “Sababu za Kuwa na Tumaini,” iliniimarisha. Ningependa kuwapatia watu wengi kadiri niwezavyo gazeti hilo.

Y. N., Japani

Mimi hushtuka ninapopatwa na jambo fulani baya. Lakini makala hizo zilijibu sala zangu! Hatua za kushinda maoni mabaya zilikuwa wazi sana hivi kwamba huwa rahisi sana kwangu kufuata hatua hizo ninapokuwa na maoni mabaya. Mimi huweka gazeti hilo kando ya kitanda changu na kulitazama kila siku.

S. T., Japani

Ndege Wanaojisafisha Ndege wanaojisafisha huonekana sana mahali ninakoishi. Niliposoma makala yenye kichwa “Je, Wanataka Tu Kujirembesha?” (Aprili 22, 2004), nilielewa faida ambazo ndege hupata wanapojisafisha. Ninataka kuwashukuru kwa makala hiyo yenye kuelimisha kuhusu viumbe wa pekee wa Mungu.

F. K., Nigeria

Mimi hufurahia sana kusoma makala kuhusu mimea, wanyama, na ndege. Katika makala hiyo kuhusu ndege nilijifunza kwamba wasipojisafisha wanaweza kufa. Sijawahi kufikiria jambo hilo.

K. G., Urusi

Disko Asanteni sana kwa makala yenye kichwa “Vijana Huuliza . . . Vipi Kwenda Disko?” (Aprili 22, 2004) Ninakubali kwamba Wakristo hawapaswi kwenda disko. Ninasikitika kwamba sikumjua Yehova zamani wakati nilipokuwa nikienda disko.

L., Indonesia

Kusema kweli, nimewahi kwenda mahali ambapo sikupaswa kwenda. Ninapenda kucheza dansi, na kila wakati nilijitetea. Baadaye mimi huhisi hatia, si kwa sababu ya kufanya jambo lolote baya bali kwa sababu ya mwenendo mbaya wa watu niliokuwa nao kwenye disko! Makala hiyo ilifichua ukweli kuhusu disko, yaani disko nyingi ni hatari na zenye ukosefu wa adili.

D. K., Australia