Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Nini Kuna Dini Nyingi Sana?

Kwa Nini Kuna Dini Nyingi Sana?

Kwa Nini Kuna Dini Nyingi Sana?

Mwanamke mmoja aliiandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Guatemala, na kueleza kuhusu mazungumzo yake na Shahidi fulani walipokuwa wakisafiri kwa basi. Mwanamke huyo alisema hivi: “Tulizungumzia kile kinachosababisha kuwe na dini nyingi sana.” Kisha alieleza kwamba Shahidi huyo alitoa broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? na kufungua somo lenye kichwa “Unaweza Kuipataje Dini ya Kweli?” Mwanamke huyo aliandika hivi: “Somo hilo lilinishangaza. Hapo ndipo nilipotambua kwamba lazima kuwe na kikundi kimoja tu cha waabudu wa kweli.”

Aliposoma broshua hiyo alipendezwa sana. Anaeleza hivi: “Ninaandika ili nijue ikiwa mnaweza kunisaidia kujifunza Biblia kwa kutumia broshua hii kwa sababu nina uhakika kwamba ina ukweli.”

Broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? iliyo na kurasa 32 ina ukubwa kama wa gazeti hili. Zaidi ya habari iliyotajwa juu, broshua hiyo inajibu maswali kama vile:

▪ Mungu ni nani?

▪ Ni nini kusudi la Mungu kwa dunia?

▪ Ufalme wa Mungu ni nini?

▪ Unawezaje kuwa na maisha ya familia yenye furaha?

Wewe pia unaweza kufaidika kwa kusoma broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.