Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Jarida Ambalo Huongozwa na Mungu’

‘Jarida Ambalo Huongozwa na Mungu’

‘Jarida Ambalo Huongozwa na Mungu’

MWANAMUME fulani anayejifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova huko Nigeria alihudhuria semina iliyopangwa na kamati moja ya Afrika inayoshughulikia masuala ya wanawake na watoto. Alienda huko akiwa na magazeti mawili ya karibuni ya Amkeni!

Siku ya kwanza ya semina hiyo, mwanamume huyo alitambua kwamba msemaji alikuwa akitumia habari iliyokuwa katika mojawapo ya magazeti hayo. Kichwa cha gazeti hilo kilikuwa “Uhai Una Thamani.” (Oktoba 22, 2001) Kwa hiyo alichukua gazeti lake na kuanza kufuatana na msemaji.

Mwishoni mwa siku hiyo, wakili mmoja ambaye angetoa hotuba siku iliyofuata aliona kichwa cha gazeti hilo jingine la Amkeni! ambalo mwanafunzi huyo wa Biblia alikuwa nalo. Lilikuwa na mfululizo wenye kichwa “Msaada kwa Wanawake Wanaopigwa.” Wakili huyo aliomba gazeti hilo. Usiku huo aliacha hotuba aliyokuwa ametayarisha na kuanza kutayarisha hotuba mpya akitumia makala zilizo katika gazeti hilo la Amkeni! Siku iliyofuata, wakili huyo alipokuwa akitoa hotuba yake, mwanamke aliyekaa karibu na yule mwanafunzi wa Biblia alitoa gazeti lake la Amkeni! na kufuatana naye.

Mwanafunzi huyo wa Biblia alichangia kwa njia muhimu mazungumzo katika semina hiyo kwa sababu ya kusoma makala za Amkeni! Alisema hivi: ‘Sina shaka kwamba jarida la Amkeni! huongozwa na Mungu.’

Je, ungependa kuletewa jarida hilo nyumbani kwako kwa ukawaida? Kwa nini usimwulize Shahidi wa Yehova akufanyie mpango?