Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Tunapaswa Kulitumia Jina la Mungu?

Je, Tunapaswa Kulitumia Jina la Mungu?

Je, Tunapaswa Kulitumia Jina la Mungu?

MNAMO 1902, jarida moja (The Presbyterian and Reformed Review) liliripoti kutolewa kwa tafsiri ya Biblia ya American Standard ya mwaka wa 1901, ambayo ni tafsiri iliyosahihishwa ya King James Version ya karne ya 17. Katika makala hiyo, jarida hilo lilisema kwamba inafaa kutumia jina la Mungu, Yehova, kila mahali katika Biblia ya Kiingereza:

“Hatuelewi kwa nini kuwe na tofauti ya maoni kuhusu kufaa kwa hatua hiyo. Hili ni jina la kibinafsi la Bwana, ambalo amechagua litumiwe na watu Wake: hasara ambayo imetokana na kutumia majina ya heshima badala yake ni kubwa sana. Ni kweli kwamba kuna maoni tofauti kuhusu jinsi linavyopaswa kutamkwa, na hakuna yeyote anayeamini kwamba linapaswa kutamkwa ‘Jehovah.’ Hata hivyo, jina hilo ni muhimu kwa msomaji wa Kiingereza kwa kuwa linatambuliwa kuwa jina la Mungu; na ungekuwa ushupavu tu kutumia Yahwé badala yake au miundo mingine inayotumiwa leo na waandishi wasomi ambayo huenda iwe au isiwe sahihi sana. Tunaiona kuwa faida kubwa kwa msomaji wa Kiingereza wa Agano la Kale kwamba kwa mara ya kwanza ataliona jina ‘Jehovah’ katika tafsiri yake anayoipenda na kujifunza yote ambayo ‘Jehovah’ amekuwa na ambayo amewafanyia watu Wake.”

Tafsiri nyingine nyingi za Biblia za Kiingereza zinalitumia jina “Jehovah” au muundo mwingine wa jina la Mungu. Vivyo hivyo, jina la Mungu linapatikana katika tafsiri nyingi zisizo za Kiingereza. Mifano kadhaa inaonyeshwa katika ukurasa huu. Mungu alimwambia Musa hivi kuhusu jina lake, Yehova: “Hilo ndilo jina langu mpaka wakati usio na kipimo, na huo ndio ukumbusho wangu kwa kizazi baada ya kizazi.” Kwa kweli, basi, hakuna shaka yoyote kwamba jina la Mungu linapaswa kutumiwa leo!—Kutoka 3:13-15.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Andiko la Zaburi 83:18 linavyoonekana katika lugha mbalimbali

Kitsonga

Kishona

Kivietnam

Kihispania

Kihindi

Kitagalog

Kiingereza