Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Ulaghai Ningependa mjue kwamba nilithamini sana mfululizo wenye kichwa “Jilinde Dhidi ya Ulaghai.” (Julai 22, 2004) Nina biashara ndogo ambayo mimi hufanyia nyumbani, na nimewahi kulaghaiwa. Hisia nilizokuwa nazo zilikuwa tu kama zile zinazoelezwa katika mfululizo huo. Nilihisi aibu na hatia kwa sababu ya kuwa mjinga. Nilifuata mapendekezo yaliyotolewa na mfululizo huo. Nilikubali makosa yangu, nikasali kwa Yehova, na kuzungumza na mzee ambaye ni rafiki yangu. Kwa msaada wa makala hizo, nimejitahidi kushughulikia jambo hilo. Hicho ni kitulizo kwelikweli!

T. G., Marekani

Ngono Kabla ya Ndoa Makala yenye kichwa “Vijana Huuliza . . . Kuna Ubaya Gani Kufanya Ngono Kabla ya Ndoa?” iliniimarisha sana. (Julai 22, 2004) Maoni yaliyotolewa na vijana wanaotajwa katika makala hiyo yalikuwa sawa na yale ambayo mimi nimekuwa nayo. Maneno yaliyonipendeza hasa yalikuwa yale ya Zaburi 84:11, ambayo inatuambia kwamba Yehova hatawanyima jambo lolote jema wale wanaotembea bila kosa.

T. U., Ujerumani

Nikiwa kijana, nyakati zote nimejaribu kufanya yale ninayoweza ili nidumu nikiwa safi kiadili machoni pa Yehova, lakini nyakati nyingine ni vigumu kufanya hivyo. Makala hiyo ilinitia moyo sana na kunikumbusha kwamba si mimi tu ninayepatwa na magumu kutoka katika ulimwengu wa Shetani. Inatia moyo sana kujua kwamba Yehova anawajali sana vijana.

F. B., Botswana

Sura Ningependa kuwashukuru kwa makala yenye kichwa “Kuhangaikia Sura Kupita Kiasi.” (Julai 22, 2004) Nina umri wa miaka 21, nami nilihangaika sana kwa sababu nilikuwa mkubwa kuliko watu wengine. Sasa ningependa kudumisha urembo wa mtu wa ndani. Ni kama makala hiyo iliandikwa kwa ajili yangu!

N. U., Japani

Ni jambo la kusikitisha kwamba siku hizi tunaathiriwa na maoni ya kwamba tunapaswa kuwa na mwili usio na kasoro. Nyakati nyingine hilo huwa kama pigano na mara nyingi mimi husikitika kwamba ninalemewa. Ningependa kufanya maendeleo, na makala hiyo ilinisaidia sana kufanya hivyo!

D. P., Ujerumani

Kuugua Tena Polio Asanteni sana kwa masimulizi ya Jack Meintsma yaliyokuwa katika makala yenye kichwa “Ugonjwa Unaporudi Mara ya Pili.” (Julai 22, 2004) Nimeugua polio kwa miaka 23 iliyopita lakini nina dalili kama zile zinazotajwa katika makala hiyo. Ningependa kumshukuru Ndugu Meintsma kwa habari aliyotoa kuhusu vifaa vinavyosaidia na kuhusu kutotumia sana misuli iliyoathiriwa.

U. K., Austria

Niliugua polio nilipokuwa na umri wa miaka miwili na nusu kisha ukarudi tena nilipokuwa na miaka 25. Madaktari hawakufahamu vizuri ugonjwa huo, nao walikabili hali ngumu walipojaribu kuutibu. Kabla ya kusoma makala hiyo sikuwa nimepata habari nyingi hivyo kuhusu ugonjwa huo.

J. E., Ufaransa

Mama yangu alipatwa na ugonjwa wa polio nilipokuwa na miaka sita. Maelezo ya wazi kuhusu ugonjwa huo yamenisaidia kuelewa hali yake.

T. V., Italia

Nilianza kuugua polio nilipokuwa na umri wa miezi 18, lakini sijaathiriwa sana kama Ndugu Meintsma. Hata hivyo, sina nguvu nyingi kwa sababu misuli yangu ni dhaifu. Makala hiyo ilinisaidia kufahamu jinsi ninavyoweza kuhifadhi nguvu zangu. Faida kubwa zaidi niliyopata kutokana na makala hiyo ilikuwa kusoma kwamba Yehova anaona, naye anajali!

L. J. Marekani