Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mambo ya Kurudia na Familia

Mambo ya Kurudia na Familia

Mambo ya Kurudia na Familia

WATOTO wengi huthamini sana magazeti ya Amkeni! Mvulana mwenye umri wa miaka tisa aliandika hivi: “Asanteni sana kwa makala nzuri sana. Endeleeni kuandika magazeti haya yenye kupendeza.” Baada ya kusoma makala kuhusu pomboo katika gazeti la Januari 8, 2002, msichana mmoja aliandika hivi: “Kiangazi kilichopita nilipokuwa na umri wa miaka saba, pomboo watatu walikuja na kututazama tulipokuwa tukiogelea, kama tu wale katika makala niliyosoma walivyofanya. Mimi hupenda kuona vitu vya ajabu ambavyo Yehova ameumba. Asanteni kwa makala ambazo nyinyi huchapisha!”

Je, wazazi mnaweza kuwaonyesha watoto wenu makala katika toleo hili la Amkeni! ambazo zitawanufaisha? Labda watafurahia kujibu maswali yafuatayo.

Tafuta picha hizi katika gazeti hili kisha ujibu maswali yafuatayo

1. Ni nini kilichompata shomoro huyu, naye alisaidiwaje?

2. Yesu alisema nini kuhusu shomoro?

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

1. Mnyama huyu anaitwaje, na ni nani aliyemuumba?

2. Mnyama huyu anaweza kufanya mambo gani ya ajabu?

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

1. Msichana huyu alichagua kichwa gani kwa ajili ya mgawo wa somo la historia waliopewa, na kwa nini?

2. Unaweza kuwaelezaje wengine kumhusu Yehova?

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 31]

Benjam Pöntinen