Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Vijana Wanatafuta Majibu

Vijana Wanatafuta Majibu

Vijana Wanatafuta Majibu

Katika mwaka wa 2002 wakati Siku ya 17 ya Vijana Wakatoliki Ulimwenguni ilipoadhimishwa huko Toronto, Kanada, mamia ya maelfu ya watu walikuja kutoka sehemu zote za dunia. Ingawa Mashahidi wa Yehova hawakuhusika, walitazamia vijana wengi wangekuja jijini. Walijitayarishaje? Kama Wakristo wa karne ya kwanza, walitumia fursa hiyo kuzungumza nao kuhusu Biblia.—Matendo 16:12, 13.

Mashahidi waliwapongeza vijana hao kwa kupendezwa na mambo ya kiroho. Hilo lilifanya wawe na mazungumzo mengi ya Biblia na ya kirafiki. Msichana mmoja alipoulizwa na Shahidi fulani ikiwa hiyo Siku ya Vijana Ulimwenguni ilikuwa kama alivyotarajia, alisema hivi: “Kufikia sasa kumekuwa na muziki na kucheza dansi, lakini hakuna jambo ambalo limeimarisha imani yangu.”

Shahidi huyo alimpa msichana huyo broshua yenye kichwa Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, na kumweleza kwamba broshua hiyo ina majibu ya maswali mengi ambayo watu wengi wameuliza kuhusu Biblia, kama vile, “Je, kweli ni Neno la Mungu?” na “Tunawezaje kujua kwamba haijabadilika tangu wakati ilipoandikwa?”

Msichana huyo akasema: “Hayo ndiyo maswali ambayo hunisumbua. Ninahitaji majibu kwa maswali yangu. Ninataka kuisoma sasa hivi. Labda yale nitakayosoma ndiyo mambo muhimu zaidi nitakayopata katika safari hii.”

Hayo ni mfano tu wa mazungumzo ambayo Mashahidi walikuwa nayo na watu waliohudhuria hiyo Siku ya Vijana Wakatoliki Ulimwenguni. Ikiwa wewe pia ungependa kupata nakala ya broshua hiyo yenye kurasa 32 ambayo ina kichwa Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, jaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.