Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Akina Baba Nimemaliza kusoma mfululizo wenye kichwa “Sifa za Baba Mzuri.” (Agosti 22, 2004) Ninabadili ratiba yangu ya kazi ili niwe na wakati mwingi zaidi wa kushughulikia madaraka ya familia na ya kutaniko. Ninapofikiria hali yangu ya kiuchumi, nyakati nyingine nimehisi ninapaswa kufanya kazi zaidi ili nipate pesa nyingi zaidi. Lakini mfululizo huo ulinisadikisha kuwa wakati ninaotumia na familia yangu ni muhimu kuliko pesa. Nilitiwa moyo na masimulizi ya akina baba waliofanikiwa.

K. S., Japani

Mimi na dada yangu tulithamini sana mfululizo huo. Sisi huzungumza mara chache sana na baba yetu. Tunampenda na ingawa hatuaambii, tunajua kuwa anatupenda. Kusoma makala hizo kulifanya tuhisi kuna mtu anayetuelewa. Tunawashukuru sana!

V. D., Italia

Umashuhuri Makala yenye kichwa “Kitu Bora Kuliko Umashuhuri wa Ulimwengu” (Agosti 22, 2004) ilijibu sala zangu. Ilinisadikisha kwamba nilifanya uamuzi unaofaa kurudia kazi ya kuhubiri ya wakati wote. Kama makala hiyo ilivyoonyesha, mwanzoni baba ya Charles hakukubaliana na uamuzi wake. Lakini alithawabishwa sana baadaye! Ninatumaini mama yangu atakubaliana na uamuzi wangu wa kupanua utumishi wangu kwa Yehova. Asanteni kwa kutueleza kuhusu watumishi waaminifu wa Yehova kupitia makala kama hizo.

Y. P., Ukrainia

Nikiwa kijana, nyakati nyingine mimi hukengeushwa na ulimwengu na vitu vyake vyenye kuvutia. Kwa kweli, kazi ya kimwili niliyochagua ingenifanya mashuhuri. Niliposoma makala hiyo, nilitambua kwamba sikuchagua kazi ili nimtumikie Yehova. Niliguswa moyo sana na masimulizi ya Ndugu Charles Sinutko kwa sababu ingawa alikuwa mashuhuri, alichagua kumtumikia Yehova. Makala hiyo ilinionyesha kwamba hakuna jambo bora ulimwenguni kuliko kumtumikia Yehova wakati wote.

R. K., Kanada

Nilivutiwa kwamba Ndugu Sinutko alikataa kazi nzuri sana ya kuimba ili amtumikie Yehova wakati wote. Mimi na mume wangu tunafurahia sana utumishi wa upainia. Tunataka kufuata mfano wa Ndugu Sinutko kwa kuweka imani katika Yehova na kutanguliza Ufalme wa Mungu maishani mwetu. Asanteni kwa kuchapisha masimulizi hayo yenye kujenga!

E. S., Japani

Ngono Kabla ya Ndoa Ningependa kuwashukuru kwa makala yenye kichwa “Vijana Huuliza . . . Ninawezaje Kuepuka Kufanya Ngono Kabla ya Ndoa?” (Agosti 22, 2004) Mimi ni mwalimu na mshauri, kwa hiyo nilipendezwa sana na makala hiyo. Wakati wa mazungumzo darasani, nilitaja mambo fulani ambayo yangewasaidia wanafunzi waonwe na Yehova Mungu kuwa watakatifu na wanaostahili sifa, na wafanye maendeleo mazuri katika masomo yao bila kukabiliana na matatizo yanayotokea kwa kufanya ngono kabla ya ndoa. Wanafunzi wengi walipendezwa na walitaka kujifunza mengi zaidi kuhusu Biblia! Walimu fulani wameniomba nizungumze na wanafunzi katika madarasa yao. Kila juma, mimi hukutana na wanafunzi wa darasa langu kuzungumzia habari mbalimbali kutoka kitabu Vijana Huuliza.

B. C., Msumbiji

Nina miaka 25, nami nimejitahidi sana kubaki nikiwa bikira. Sasa nimetiwa moyo hata zaidi kuingia katika ndoa yenye kuheshimika. Endeleeni na kazi yenu nzuri.

F. K., Uganda