Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoweza Kuzaa Hata ingawa sijasoma sana kuhusu tiba, nilifurahia kusoma makala zenye kichwa, “Matibabu ya Kutoweza Kuzaa na Masuala Yanayohusika.” (Septemba 22, 2004) Inapendeza kutambua jinsi Yehova anavyothamini sana uhai wa wanadamu. Maelezo ya wazi kuhusu masuala yanayohusika humsaidia mtu amtumaini zaidi. Watu wengi katika eneo la kutaniko letu wamependezwa kupokea gazeti hilo.

V. P., Urusi

Mimi na mume wangu tumejaribu kupata watoto tangu tulipooana. Sasa, miaka kadhaa baadaye, tunakabili masuala yaliyofafanuliwa katika makala hizo. Inatia moyo sana kujua kwamba Yehova hutoa chakula kwa wakati unaofaa. Inahuzunisha sana kuambiwa kwamba huwezi kupata mtoto. Lakini kupitia utafiti na kupitia makala hiyo, nimefarijika kujua kwamba wengine pia hupatwa na tatizo hilo. Tunaona ni baraka kubwa kwamba tunaweza kutumia wakati wetu kumtumikia Yehova kikamili.

T. O., Marekani

Vitiligo Asanteni sana kwa makala yenye kichwa, “Vitiligo Ni Nini?” (Septemba 22, 2004) Nimekuwa na ugonjwa huo kwa miaka mitano. Lakini nimeweza kukabiliana nao vizuri zaidi baada ya ninyi kuchapisha makala hiyo. Ninafurahi sana kuwa katika tengenezo la Kikristo linalojali kila mmoja wetu!

C. H., Ujerumani

Nimekuwa nikiugua vitiligo kwa miaka kadhaa. Bila kutia chumvi, ugonjwa huo huathiri sana akili na hisia. Yehova anatufundisha tufikirie zaidi hisia za wengine. Ninatazamia kwa hamu wakati ambapo rangi ya ngozi yangu itarudi.

B. W., Marekani

Nimekuwa nikiugua vitiligo kwa miaka 25. Inafariji sana kufahamu kwamba wengine pia hufadhaika kama mimi. Watu wengi wana maoni yasiyofaa kuhusu ugonjwa huo, lakini makala hiyo itawasaidia wauelewe vizuri zaidi. Asanteni sana kwa kuzungumzia habari hiyo!

K. S., Japani

Nimekuwa na tatizo hilo kwa miaka 30 hivi. Nilipokuwa mtoto, nilifanyiwa mzaha na marika wangu kwa sababu ya sura yangu. Nimejifunza kukabiliana na ugonjwa huo. Kama Sibongile, nimeamua kuwatia wengine moyo kwa kuwaeleza ahadi ya Biblia kwamba karibuni Yehova ataondoa matatizo yote ya afya na mahangaiko ya kihisia ambayo hutokeza uchungu mwingi sana.

J. M., Jamhuri ya Cheki

Binti yangu mwenye umri wa miaka 19 ana ugonjwa huo. Amelia na kusali mara nyingi sana kwa Yehova kuhusu ugonjwa huo. Anampenda Yehova na hivi karibuni amekuwa mhubiri wa wakati wote. Tunashukuru sana kwamba mnachapisha makala kama hizo kwani zinatusaidia kuhisi kwamba Yehova anatujali.

S. S., Japani

Mimi ni mhubiri wa wakati wote. Siwezi kueleza jinsi ninavyohisi watu wanaponitazama na wanaposita kunisalimu kwa mkono au kunikumbatia kwa sababu rangi ya ngozi yangu imeharibika. Nilifarijika sana kupata makala hiyo sahihi na yenye upendo. Asanteni kwa kuwaonyesha wengine kwamba ugonjwa wetu hauambukizwi na kwa kutuonyesha kuwa Yehova anatujali.

C. S., Marekani