Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Wasichana Wanaopata Mimba Niliguswa moyo na ule mfululizo wa makala, “Wasichana Wanaopata Mimba—Tatizo la Ulimwenguni Pote.” (Oktoba 8, 2004) Nilipata mimba nilipokuwa na umri wa miaka 16. Ninashukuru kwamba mlikazia umuhimu wa kumsaidia mama na kwamba Yehova humjali mtoto asiye na hatia. Asanteni kwa makala hiyo yenye upendo.

M. R., Marekani

Nilimpa mkuu wa wakunga kwenye kliniki ya hapa gazeti hilo la Amkeni! Alisema kwamba wasichana wengi wenye umri wa miaka 14 na 15 wanapata watoto, jambo ambalo halikuwepo hapa zamani. Alisema kwamba angependa nakala 20 za gazeti hilo mara moja ili awape vijana na wazazi wao.

I. R., Benin

Niligundua kwamba nina mimba mwezi mmoja kabla sijafikisha umri wa miaka 17. Hilo ndilo lilikuwa jambo gumu zaidi na lenye kuvunja moyo zaidi ambalo nimewahi kuwaambia wazazi wangu. Ninatumaini kwamba vijana watasoma makala hiyo na kuichukua kwa uzito. Sikufikiri kamwe kwamba ningeweza kupatwa na jambo hilo!

D. C., Marekani

Nilipata mtoto nilipokuwa na umri wa miaka 17. Nililazimishwa kufunga ndoa ambayo ilivunjika upesi. Mimi huhuzunika ninapofikiria jinsi nilivyopoteza fursa ya kutimiza mambo mengi katika miaka hiyo kwa sababu tu ya kufanya ngono kabla ya ndoa bila kujua matokeo. Sikuzote mimi hujaribu kuwashauri vijana wasifanye kosa hilo zito. Nawashukuru kikweli kwa ajili ya makala hiyo!

N. C., Honduras

“Yehova, Umenipata!” Nina umri wa miaka 15, na nilifurahia sana kusoma makala yenye kichwa, “Yehova, Umenipata!” (Oktoba 8, 2004) Simulizi la Nelly lilinisaidia kuelewa kabisa maneno haya ya Yakobo 4:8: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” Asanteni kwa makala hiyo yenye kuimarisha imani!

K. P., Marekani

Simulizi la Nelly Lenz linatusadikisha kwamba Yehova ni Mungu mwenye upendo, na kwamba atatusaidia tumpate ikiwa tutaendelea kumtafuta.

M. K., Japani

Inafariji kupata uhakikisho kupitia makala kama hizo kwamba Yehova huwaona kondoo wake wote kuwa wenye thamani sana hivi kwamba anawakumbuka mahali popote walipo na kutegemeza kila mmoja wao.

J. G., Kanada

Makala hiyo ilifanya nidondokwe na machozi. Wazazi wangu si Mashahidi wa Yehova, nao walinisumbua sana. Ninafurahi kwamba Nelly alidumisha azimio lake la kumtumikia Yehova.

K. L., Jamaika

Nina umri wa miaka 12. Inatia moyo sana kujua kwamba hata uwe na matatizo mengi kadiri gani nyumbani, sikuzote Yehova hukusaidia kukabiliana nayo.

J. W., Marekani

Nelly alifanya vizuri kutusimulia mambo yaliyompata maishani. Simulizi hilo litawasaidia watoto wanaokabili hali kama hizo. Na watu wazima wanapaswa kukumbuka watoto hao. Ni rahisi kusahau kwamba wana mahitaji ya pekee kutanikoni.

M. K., Denmark

Sijawahi kuguswa moyo hivyo na simulizi lingine. Ninajua jinsi ilivyo vigumu kwa kijana kutetea kweli akiwa peke yake. Kwa miaka minne ni mimi tu niliyekuwa nikimtumikia Yehova. Niliguswa moyo sana kusoma kuhusu jinsi Yehova alivyomtunza Nelly. Asanteni kwa simulizi hilo lenye kujenga. Asante Nelly!

G. W., Ujerumani