Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jinsi ya kuwa rafiki ya Mungu

Jinsi ya kuwa rafiki ya Mungu

Jinsi ya kuwa rafiki ya Mungu

▪ Broshua Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! yenye kurasa 32 hutufundisha jinsi ya kuwa rafiki ya Mungu. Ina masomo yenye kupendeza kama vile, “Mungu Anataka Uwe Rafiki Yake” na “Mungu Ndiye Rafiki Bora Uwezaye Kuwa Naye.” Broshua hiyo imekusudiwa imsaidie msomaji ajifunze mafundisho ya msingi ya Biblia.

Katika somo lake, “Rafiki za Mungu Wataishi Katika Paradiso,” broshua hiyo inaonyesha waziwazi kusudi la Mungu kwa dunia. Hata hivyo, ili tuishi katika Paradiso ambayo Biblia inaahidi, ni lazima tujifunze jinsi ambavyo Mungu anataka tumtumikie. Masomo kama vile, “Jinsi ya Kupata Dini ya Kweli” na “Ikatae Dini Isiyo ya Kweli!” yatakusaidia uwe rafiki ya Mungu na upate kibali chake. Tuna hakika kwamba utafurahia kusoma broshua hiyo.

Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea broshua Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! bila malipo.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.