Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Watoto Hivi karibuni nilisoma mfululizo wa makala yenye kichwa, “Wazazi Wanapaswa Kufanya Nini Mtoto Akiwa Mchanga?” (Oktoba 22, 2004) Nilipendezwa sana na makala hizo hivi kwamba nikaamua kuwaandikia. Binti yangu atafikisha umri wa miaka mitano hivi karibuni. Nilifikiri kwamba nilihitaji kumpangia mambo ya kufanya kila wakati. Hata hivyo, gazeti hilo lilisema kuwa walimu fulani walihisi kwamba kuacha mtoto acheze kama kawaida humchochea kubuni mambo na kusitawisha uwezo wa kuchangamana na watu, ustadi wa kiakili na wa kihisia. Asanteni sana! Tafadhali endeleeni kuchapisha makala kama hizo!

I. K., Urusi

Nilitokwa na machozi niliposoma makala hizo. Nilikumbuka miaka 29 iliyopita nilipopata mtoto wangu nikiwa mama mchanga asiyemjua Yehova. Nilikosea mara nyingi. Lakini machozi yangu ya majuto yaligeuka kuwa machozi ya furaha. Binti yangu alijifungua mtoto wake wa kwanza juma lililopita. Ninamshukuru sana Yehova kwamba mjukuu wangu ana wazazi wanaompenda Yehova na ambao watanufaika na makala hizo.

E. H., Marekani

Vijana Huuliza Asanteni sana kwa makala “Vijana Huuliza . . . Nitamwambiaje Jinsi Ninavyohisi?” (Oktoba 22, 2004) Hivi karibuni, mwanamke mmoja kijana alivunja uchumba wetu. Kwa kuwa nilikuwa bado nampenda, nilitarajia kwamba atabadili uamuzi wake. Lakini baada ya kusoma makala hiyo, nilitambua kwamba hiyo ilikuwa ndoto tu, na kuanzia hapo nikakubali ukweli wa mambo. Asanteni sana kwa kuzungumzia habari hiyo. Kwa mara nyingine tena, naona jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kutusaidia.

Y. K., Japani

Hata ingawa kwa sasa sina nia ya kumjua mtu fulani nikiwa na kusudi la kufunga ndoa, makala hiyo inanifaidi kwa kuwa inanisaidia nijihadhari. Ni kweli kwamba sisi vijana hushambuliwa na Shetani kwa urahisi, lakini ni kweli pia kwamba Yehova hutusaidia. Endeleeni kuchapisha makala kama hizo!

C. D., Rumania

Makala hiyo ilinisaidia kuona mambo kwa njia halisi. Ilinifanya niazimie kutoeleza hisia zangu haraka. Zaidi ya yote, ilinitia moyo nifanye mengi katika kutaniko ili niwe na sifa nzuri na niboreshe uhusiano wangu na Yehova. Jambo hilo litafanya nipendwe zaidi na watu wote. Asanteni sana kwa kuwajali vijana kwa njia hiyo!

D. K., Uholanzi

Siku moja rafiki yangu alikuwa akinieleza kuhusu mtu fulani ambaye yeye alipendezwa naye. Alitaka mashauri yangu. Tulijaribu kufikiria kanuni za Biblia ambazo zingemsaidia. Tulishangaa sana tulipopokea gazeti hilo siku iliyofuata. Asanteni sana kwa kuchapisha makala kama hizo!

J. S., Ireland

Nina umri wa miaka 14. Wanadarasa wenzangu hupenda kuzungumza kuhusu mahaba na mahusiano na watu wa jinsia tofauti. Niliposoma makala hiyo, nilijifunza mengi kuhusu jinsi ya kutafuta mwenzi wa ndoa wakati ujao. Pia nilielewa jinsi Yehova hutujali sana na kutupa mashauri mazuri. Ninataka kutenda kwa hekima, katika njia itakayompendeza Mungu ninapokuwa na watu wa jinsia tofauti. Tafadhali endeleeni kuchapisha makala nzuri kama hizo.

K. I., Japani