Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Makala ya Zamani Yagusa Mioyo ya Wengi

Makala ya Zamani Yagusa Mioyo ya Wengi

Makala ya Zamani Yagusa Mioyo ya Wengi

KATIKA shule moja huko Suwałki, kaskazini-mashariki ya Poland, mwalimu aliwaambia wanafunzi watayarishe mjadala kuhusu utoaji-mimba. Justyna, mwenye umri wa miaka 16 alitafuta habari kutoka kwenye vichapo vya Mashahidi wa Yehova. Siku ya mjadala huo, mwalimu aliwapa wanafunzi nafasi watoe maoni yao.

Justyna anaeleza hivi: “Nilimwendea mwalimu na kumwonyesha makala yenye kichwa, ‘Diary of an Unborn Child,’ iliyochapishwa katika toleo la Kiingereza la Amkeni!, Mei 22, 1980.” Alimwambia hivi mwalimu wake: “Tafadhali ona kwamba makala hii inaeleza maoni ya mtoto, kijusi ambacho kitauawa. Nafikiri inapendeza.” Mwalimu alianza kusoma makala hiyo kwa sauti. Wanafunzi walinyamaza na kusikiliza kwa makini.

Kabla hata hajafika katikati ya makala hiyo, mwalimu alishindwa kujizuia na akamwomba mwanafunzi mmoja aendelee kusoma. Mwalimu aliketi chini na kuanza kulia. Baada ya makala hiyo kusomwa, kulikuwa na mazungumzo yenye kupendeza na baadhi ya wanafunzi waliomba nakala ya makala hiyo. Justyna anasema hivi: “Wanafunzi walibadili maoni yao kuhusu vichapo vya Mashahidi wa Yehova. Hapo zamani walikuwa na maoni yasiyofaa, lakini sasa wana maoni mazuri. Mvulana mmoja hata husoma magazeti ya Amkeni! kwa ukawaida sasa.”

Kama Justyna aliyetumia kwa matokeo makala iliyokuwa katika toleo la gazeti la Amkeni! lililochapishwa zaidi ya miaka 20 iliyopita, wewe pia unaweza kupata “mfuko uliojaa hekima” katika matoleo ya zamani ya gazeti hilo. (Ayubu 28:18) Unapohudhuria mikutano katika Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova lililo karibu nawe, unaweza kuchunguza mabuku yaliyojalidiwa ya Amkeni! yaliyo katika maktaba. Utafurahia kusoma makala zenye kunufaisha ambazo hazipotezi thamani hata baada ya muda kupita. Unaweza pia kupata toleo la karibuni la Amkeni! kutoka kwa Mashahidi wa Yehova mahali unapoishi.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Justyna alipokuwa shuleni