Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Vijana Huuliza Asanteni kwa makala nzuri yenye kichwa, “Vijana Huuliza . . . Nifanyeje Nisipofanikiwa?” (Novemba 22, 2004) Kama Ana, nilihisi nilikuwa nimemkosea Mungu naye hangenisamehe. Lakini makala hiyo ilieleza kwamba Yehova alimsamehe Daudi na kumtegemeza licha ya udhaifu wake. Inatia moyo sana kujua kwamba hata tukianguka, Yehova atatusaidia kusimama tena!

G. C., Italia

Andiko la Wagalatia 6:4 lilinisaidia sana. Nilitambua kwamba nyakati zote mimi hujilinganisha na wanafunzi bora darasani. Makala hiyo ilinisaidia kuelewa kwamba ninajiumiza tu.

C. C., Ufaransa

Shambulizi la Magaidi Makala “Kupambana na Mfadhaiko Baada ya Shambulizi la Magaidi,” ilinigusa moyo sana. (Novemba 8, 2004) Masimulizi hayo yalikuwa yenye kutia moyo. Nilijifunza kwamba tunaweza kuimarishwa kwa kukumbuka maandiko na kuwa na tumaini hakika la Paradiso. Ni muhimu kuweka maandiko mengi iwezekanavyo moyoni.

I. A., Japani

Nilivutiwa sana kuona kwamba ingawa akina ndugu walikuwa wamejeruhiwa, walifikiria Biblia na tumaini ambalo Yehova anatupa. Ningependa kutembelea Hispania siku moja na kuwaeleza akina ndugu jinsi walivyonitia moyo.

L. G., Marekani

Wazazi Asanteni kwa mashauri mliyotoa katika makala zenye kichwa, “Sifa za Baba Mzuri.” (Agosti 22, 2004) Sasa tunatambua jinsi ambavyo tunaweza kuelekeza moyo wa mtoto wetu kwa mambo ya kiroho ili kanuni za Yehova zikaziwe moyoni mwake tangu utotoni. Ni kana kwamba makala hizo huandikwa kwa ajili yetu hasa. Sikuzote zinatimiza mahitaji yetu ya kiroho kwa wakati wake.

K. na M. P., Poland

Wasichana Wanaopata Mimba Asanteni sana kwa mfululizo wenye kichwa “Wasichana Wanaopata Mimba—Tatizo la Ulimwenguni Pote.” (Oktoba 8, 2004) Kabla ya kumaliza kusoma mfululizo huo, nilianza kulia. Mfululizo huo ulieleza kwa usahihi mambo ambayo dada yangu anapitia. Nashukuru sana kwamba Yehova alitoa makala hizo kwa wakati wake ili zinisaidie kuelewa hisia za dada yangu.

M. S., Indonesia

Mtu anaweza kuhisi upendo na huruma za wazee wanaoonyeshwa kwenye ukurasa wa 10. Kwa kweli, picha hiyo humtukuza Yehova, mwenye upendo na rehema isiyo na kifani! Asanteni kwa kutufundisha jinsi tunavyoweza kumwiga Mungu wetu tunaposhughulika na wale ambao wamefanya dhambi nzito lakini wametubu.

T. K., Ukrainia

Kuhubiri Shuleni Nilivutiwa sana na makala “Vijana Wanaotetea Imani Yao.” (Septemba 8, 2004) Masimulizi ya Holly, Jessica, na Melissa yamenisaidia nihubiri shuleni, iwe ni kwa wanashule wenzangu au walimu. Mwanzoni niliona haya kuhubiri. Lakini sasa nimechochewa kuwahubiria wale ninaokutana nao shuleni.

G. O., Nigeria

Vitiligo Makala iliyonigusa moyo hivi karibuni ni, “Vitiligo Ni Nini?” (Septemba 22, 2004) Nimekuwa na vitiligo tangu nilipokuwa na umri wa miaka tisa. Sasa nina umri wa miaka 30 na kitu. Baada ya kupata matibabu mengi ambayo hayakufaulu, nimekubali ukweli wa kwamba nitapona kabisa katika ulimwengu mpya wa Mungu. Hata hivyo, maisha yangu yamekuwa yenye kuridhisha! Mtu anaweza kuwa na maisha yenye kuridhisha na yenye furaha licha ya ugonjwa huo wa ngozi!

M. S., Msumbiji