Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Marafiki Tangu mama yangu afe karibu miaka minne iliyopita, nimepata fursa ya kuwa na marafiki wazuri sana ninaowapenda. Makala yenye kichwa “Jinsi ya Kupata Marafiki wa Kweli” (Desemba 8, 2004) ilifanya nithamini kuwa na marafiki hao!

O. B., Marekani

Nina umri wa miaka 11, na kwa sababu fulani singeweza kupata marafiki. Baada ya kusoma makala hiyo, mambo yalibadilika na kuwa mazuri. Nilimpa gazeti hilo mwanadarasa fulani ambaye hupenda kuzungumza vibaya juu ya wengine. Tangu asome makala hizo, amejaribu kuacha tabia hiyo.

J. K., Poland

Kusoma makala hizo kulinithibitishia kwamba ninapaswa kuwa mwenye urafiki ikiwa ninataka kupata marafiki, kwamba ninapaswa kujitoa kwa wengine, kulingana na kitia moyo kinachopatikana kwenye Matendo 20:35. Mlitoa shauri zuri sana.

A. K., Poland

Nimekuwa na tatizo la kupata marafiki hata katika kutaniko la Kikristo. Sasa ninaona kwamba ninapaswa kujieleza waziwazi, kuchukua hatua ya kwanza, na kutotarajia ukamilifu kutoka kwa wengine. Kwa kweli Yehova hutupa majibu katika wakati unaofaa!

L. Z., Urusi

Kwa sababu ya matatizo kadhaa ya afya, ni vigumu kwangu kushirikiana na wengine. Niliamua kutumia habari iliyo katika makala hizo. Nilinufaishwa na shauri lililotutia moyo kuwa wanyoofu na kufunua hatua kwa hatua hisia na mawazo yetu ya kweli.

N. M., Japani

Nilizungumza na wanashule wenzangu kuhusu makala hizo wakati wa mapumziko ya mchana. Kwa sababu ya gazeti hilo, wameanza kulifahamu Neno la Mungu. Tafadhali endeleeni kuchapisha makala zinazokazia jinsi Biblia inavyoweza kuwanufaisha watu wote.

M. N., Japani

Nilifurahia sana kusoma jibu la swali lililo kwenye sanduku “Je, Mwanamume na Mwanamke Wanaweza Kuwa ‘Marafiki Tu’?” Hakuna gazeti wala kitabu ambacho kimewahi kuchapisha jibu lililo sahili na wazi kama hilo.

R. K., Ujerumani

Makala zenu husaidia sana nyakati zote. Hutusaidia kuimarisha lengo letu la kufanya mengi kwa ajili ya Yehova na kumfanya awe rafiki yetu. Asanteni sana kwa kitia moyo hicho!

R.V.H., Ujerumani

Hizi ndizo makala nilizohitaji. Nina umri wa miaka 15, nami huona ugumu wa kuanzisha urafiki. Shauri mlilotoa litanisaidia kuanzisha na kudumisha urafiki. Makala hizo zilifika wakati tu nilipokuwa nikisali kupata ushauri kuhusu namna ya kufunua hisia zangu kwa wengine.

B. E., Ufaransa

Kwa kusikitisha, hivi karibuni marafiki fulani walinikatisha tamaa, na niliteseka sana kwa kuwa nilihisi upweke. Nilitiwa moyo kujua kwamba Yehova hatuachi kamwe. Pia nilifurahia kusoma na kufuata shauri zuri kuhusu jinsi ya kupata marafiki wa kweli.

C. C., Italia

Ningependa binti yangu akue kiroho. Gazeti hilo linakazia kwamba watu wa umri wote wanaweza kuwa rafiki zako. Ninajua kwamba makala hizi zitamsaidia. Zimenisaidia.

A. L., Marekani

Ninajua kwamba ninapaswa kupendezwa na wengine na kubadili utu wangu ili niwe rafiki wa kweli. Nina uhakika kwamba Yehova atanisaidia.

M. Y., Kanada