Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Itatukia Tena?

Je, Itatukia Tena?

Je, Itatukia Tena?

TUNAPOFIKIRIA kizazi hicho, huenda tukaona kwamba kilikuwa na mambo yenye kuvutia. Kwa mfano, katika nchi za Magharibi kulikuwa na magari ya kukokotwa na farasi, watu walivaa sketi ndefu, na kofia pana. Lakini pia kilikuwa kipindi chenye kuogopesha watu walipoanza kufa kwa wingi ulimwenguni pote. Vifo hivyo vilisababishwa na nini?

Havikusababishwa na vita, ingawa wakati huo vilikuwa vimepamba moto. Tunazungumza kuhusu aina nyingine ya tauni ambayo imetajwa kuwa tauni iliyosababisha uharibifu mkubwa zaidi katika historia yote ya wanadamu, yaani, homa ya Hispania ya mwaka wa 1918-1919.

Watu waliokuwa wameambukizwa walikufa kwa wingi kwani hakukuwa na tiba inayofaa. Mamilioni ya vijana wenye afya walikufa wakiwa kati ya umri wa miaka 20 na 40. Maiti zilirundamana. Tauni hiyo ilifagilia mbali miji na vijiji fulani.

Yote hayo yalitukia zaidi ya miaka 85 iliyopita. Je, tunajua kilichosababisha tauni hiyo? Je, msiba kama huo unaweza kutukia tena? Ukitukia tena, je, tutaweza kujikinga?

Kuna jambo lingine lenye kushangaza kuhusu habari hiyo. Je, ulijua kwamba muda mrefu uliopita Biblia ilitaja kuhusu tauni ambazo zimetukia katika nyakati zetu? (Luka 21:11; Ufunuo 6:8) Je, homa ya Hispania ilikuwa sehemu ya utimizo wa unabii wa Biblia? Majibu kwa maswali hayo yatazungumziwa katika makala zinazofuata.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Watu wakijitayarisha kuwazika waliokufa kutokana na homa ya Hispania, Philadelphia, Marekani

[Hisani]

Library of the College of Physicians of Philadelphia