Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Milima—Ni Muhimu kwa Uhai Duniani (Machi 22, 2005) Kutembelea Milima ya Grand Tetons kulikuwa mojawapo ya matukio yenye kutia kicho maishani mwangu. Lakini niliposoma kuhusu umuhimu wa milima nilishangaa. Sasa ninaithamini zaidi milima iliyo duniani na Muumba mtukufu aliyeifanya.

J. G., Marekani

Ninapotazama umaridadi wa uumbaji wa Yehova, siwezi kueleza jinsi ninavyohisi. Licha ya kuharibiwa na kuchafuliwa kwa mazingira, bado tunaweza kuthamini na kufurahia milima. Ninafurahi kuwajulisha wengine yatakayotukia wakati ujao ulio karibu, kama Zaburi 72:16 inavyoahidi.

R. C., Marekani

Vijana Huuliza . . . Kwa Nini Nifanye Kazi za Mikono? (Machi 22, 2005) Mimi hufanya kazi katika kampuni ya rangi inayomilikiwa na baba yangu, lakini mtu fulani aliniambia kwamba kazi ya aina hiyo haihitaji akili nyingi. Lakini, makala hiyo ilionyesha kwamba Yesu na Paulo walifanya kazi za mikono. Sasa nimetiwa moyo sana kufanya kazi yangu kwa uchangamfu zaidi. Ningependa kujitahidi sana ili nitumie ujuzi huo katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme na ya Kusanyiko.

M. Y., Japani

Makala hiyo ilinitia moyo sana. Ilinikumbusha tena kwamba kusudi letu kuu maishani ni kumtumikia Yehova Mungu na kwamba kazi yoyote ninayochagua inapaswa kupatana na kusudi hilo. Makala hiyo yenye kupendeza ilinichochea kufanya kazi yoyote inayohitajika nyumbani. Jambo la maana zaidi ni kwamba makala hiyo ilinisaidia kujua maoni ya Yehova kuhusu kazi za mikono.

Y. K., Urusi

Minyororo ya Uhai Inayostaajabisha (Januari 22, 2005) Nina umri wa miaka 15. Tulikuwa tukijifunza kuhusu kutokezwa kwa nishati katika somo la biolojia shuleni. Nilipoenda na gazeti hilo shuleni, mwalimu wangu wa biolojia alitumia makala hiyo kufundisha, akionyesha michoro iliyokuwa katika makala hiyo. Baada ya somo hilo, kila mtu alitaka kupata gazeti lake. Makala hiyo inaonyesha wazi kwamba Yehova ana hekima nyingi sana. Bila shaka anastahili kusifiwa. Ninasubiri kwa hamu wakati ambapo uumbaji wote utamsifu Yehova!

Y. B., Urusi

“Laiti Wangejua!” (Januari 8, 2005) Nina umri wa miaka 17, nami nimefikiria mara nyingi kuhusu kuhamia eneo lenye uhitaji mkubwa wa wahubiri wa Ufalme. Mfano wa David uliimarisha azimio langu la kuhamia eneo kama hilo baada tu ya kumaliza shule. Tafadhali endeleeni kuchapisha mifano kama hiyo yenye kutia moyo. Vijana wa rika langu wanahitaji kitia-moyo cha kuendelea katika kazi ya kuhubiri.

K. O., Poland

Nina umri wa miaka 20 nami nilitokwa na machozi niliposoma makala hiyo. Niliwaza hivi, ‘ikiwa ningekufa nikiwa bado kijana, singependa kujuta kamwe kwamba sikumtumikia Yehova kwa nguvu zangu zote!’ Ningependa kuwa mtumishi wa wakati wote hivi karibuni. Nitaweka makala hiyo kwenye fremu na kuibandika ukutani ili nisisahau jinsi ambavyo nilihisi nilipoisoma. Asanteni sana kwa kuchapisha masimulizi mazuri kama hilo.

N. N., Japani