Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mtoto Anapokufa

Mtoto Anapokufa

Mtoto Anapokufa

▪ Kifo cha mtoto huwahuzunisha sana wote waliomfahamu, hasa wazazi wake. Mama fulani ambaye mwana wake mwenye umri wa miaka 16 aliteketea katika aksidenti mbaya alisema hivi kwa huzuni: “Mungu hakubali tufe badala ya watoto wetu, wala hakubali tufe pamoja nao.”

Hata hivyo, hakukata tamaa, kwani alisema hivi: “Mungu ametuambia ukweli kuhusu kifo, na hilo hufanya mimi na mume wangu tusihisi uchungu kupita kiasi au tusiwe na mawazo yasiyofaa.” Alikiri kwamba “si Mungu wetu aliyemuua mwana wetu, na Yeye anakusudia kuwafufua wafu ili waishi katika dunia paradiso. Akilini mwetu, tunaweza kumwona mwana wetu akiwa hai, mwenye afya na mwenye furaha, akiishi pamoja na marafiki na watu wa familia yake.”

Hata wale walio na tumaini hakika katika ahadi ya Mungu ya ufufuo wanahitaji faraja, kama ile ambayo mama huyo alipata kutoka kwa rafiki zake wengi. Alisema hivi: “Maandiko mengi na matendo ya fadhili ambayo walitutendea yalitoka katika broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Tuliwatia moyo marafiki wetu wote waisome ili watuelewe vizuri zaidi na huzuni ambayo tutaendelea kuwa nayo.”

Labda wewe au mtu fulani unayemfahamu atafarijika kwa kusoma broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa bila malipo.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.