Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Ni Nzuri Sana!”

“Ni Nzuri Sana!”

“Ni Nzuri Sana!”

Huko Brazili, mwalimu mmoja wa somo la jiografia alipendezwa na jinsi ambavyo gazeti Amkeni! huelimisha watu. Aliandika hivi: “Mimi hupata habari nyingi za kutumia ninapofundisha katika gazeti hilo kuliko ninazopata katika vichapo vingi ambavyo vimeandikwa kwa ajili ya walimu. Ingawa mimi ni wa dini tofauti, ninakubaliana kabisa na maadili ambayo Amkeni! hufundisha.”

Hata hivyo, mwalimu huyo alitambua kwamba Amkeni! ni mojawapo tu ya vichapo vingi ambavyo Mashahidi wa Yehova huchapisha. Aliandika: “Mwanafunzi mmoja katika darasa la sita aliniazima broshua ‘Ona Nchi Nzuri.’ Nilishangaa kuona kwamba broshua hiyo ilikuwa na habari za hali ya juu sana. Ni nzuri sana! Uwezo wa kuwazia matukio ya Biblia na kujua mahali yalipotukia hufanya kujifunza Biblia kuwe na maana, hasa kwa vijana.”

Aliongezea hivi: “Vichapo vyenu vinapatikana kila mahali: kwenye basi, miongoni mwa wanafunzi, na hata miongoni mwa watu wanaopanga foleni kwenye benki. Ninafurahi kuona kwamba vinawafikia watu wenye uhitaji ambao hawapati vichapo vyenye habari nzuri kwa urahisi. Nawapongeza kwa kazi yenu nzuri.”

Broshua ‘Ona Nchi Nzuri’ inapatikana katika lugha 80 hivi. Ina ramani na picha nyingi zenye rangi zinazoonyesha maeneo mbalimbali yanayotajwa katika Biblia, hasa Nchi ya Ahadi katika nyakati mbalimbali. Unaweza kuomba broshua hiyo yenye kurasa 36 kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea broshua ‘Ona Nchi Nzuri’ bila malipo.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Brochure covers: Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.