Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Jinsi ya Kujikinga na Kansa ya Ngozi (Juni 8, 2005) Habari iliyochapishwa katika makala hizo ni nzuri sana. Mimi ni daktari mkuu katika kliniki ya ngozi. Ningependa kupata nakala za ziada ili nizisambaze.

K. W., Denmark

Kwa sababu ya makala hiyo, niliamua kwenda hospitali ili uvimbe uliokuwa mgongoni uchunguzwe. Daktari aliniambia ungeweza kuwa aina fulani ya kansa inayoitwa Bowen. Nilipasuliwa mara moja. Makala hizo zilinisaidia kuchukua hatua haraka.

S. M., Japani

Sanduku kwenye ukurasa wa 7 lilinifanya nimwendee daktari achunguze baka fulani nililokuwa nalo. Aliniambia baka hilo lilikuwa hatua ya mapema ya kansa ya chembe za ndani za ngozi. Kama makala hiyo ilivyoonyesha, ikiwa kansa hiyo haingetibiwa mapema, ingeniua. Ninamshukuru daktari pamoja na makala hizo za Amkeni!, kwani huenda zimeokoa maisha yangu!

L. S., Marekani

Mambo ya Kurudia na Familia (Mei 8, 2005) Nilizoea kusoma makala zilizonipendeza tu, lakini baada ya kuona sehemu “Mambo ya Kurudia na Familia,” nilisoma gazeti lote ili niweze kujibu maswali yaliyokuwa katika sehemu hiyo. Punde si punde ikawa kawaida yangu kusoma gazeti lote!

Y. Z., Urusi

Nilivutiwa na ukurasa huo. Sehemu hiyo ilinifurahisha na kufanya nitambue kwamba ninahitaji kukazia uangalifu zaidi mambo ninayosoma!

D. S., Uingereza

Vijana Huuliza . . . Kwa Nini Ninavutiwa na Watu Wasiofaa? (Julai 22, 2005) Inaonekana kwamba baada ya miaka kumi ya ‘kuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana,’ bado sikujua jinsi ya kuchagua marafiki wanaofaa. (1 Wakorintho 15:58) Nilitambua kwamba sikuwa nimekomaa kihisia, lakini sikujua jinsi ningeshughulikia tatizo hilo. Namshukuru Yehova kwa makala kama hizo, ambazo hutusaidia kufanikiwa katika mfumo huu.

J. F., Marekani

Makala hiyo ilitaja kwamba ‘hatupaswi kuwapuuza kabisa watu ambao hawafahamu kweli za Biblia.’ Je, mnaweza kufafanua jambo hilo zaidi? Vipi ikiwa Mkristo ana uhusiano wa karibu na mtu asiyeamini? Je, hilo linapaswa kutuhangaisha?

D. P., Marekani

“Amkeni!” lajibu: Makala hiyo haikuwatia moyo Wakristo wafuatie uhusiano wa karibu na wasioamini. Kwa kweli, katika hali yoyote ile, kanuni hii ya Biblia inatumika: “Mashirika mabaya huharibu tabia nzuri.” (1 Wakorintho 15:33) Hata hivyo, hilo halimaanishi kwamba tunapaswa kuwapuuza kabisa watu wasioamini. Kama ilivyotajwa katika makala hiyo, Biblia inatutia moyo “tuwatendee wote mema,” si waamini wenzetu tu. (Wagalatia 6:10) Kwa kweli, utumishi wetu wa Kikristo hututaka tupendezwe kikweli na watu, tukiwatendea kwa staha na heshima. Yesu alituwekea mfano mzuri kuhusiana na hilo. Hakusitawisha kamwe uhusiano wa karibu na watu ambao hawakutaka kufanya mapenzi ya Mungu. (Yohana 15:14) Wakati huohuo, aliwaendea watu naye alijua jinsi ya kuzungumza nao na kuchangamana nao. Kwa sababu hiyo, Yesu alipata nafasi ya kutoa ushahidi mzuri. (Kwa mfano, ona simulizi kwenye Luka 7:36-50.) Kama Yesu, tuwaheshimu wasioamini. Lengo letu ni ‘kuwa wenye usawaziko, tukionyesha upole wote kuelekea watu wote.’—Tito 3:2.