Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tarehe Muhimu Zaidi Katika Historia

Tarehe Muhimu Zaidi Katika Historia

Tarehe Muhimu Zaidi Katika Historia

Ni tarehe ambayo Yesu Kristo alikufa. Kwa nini kifo cha Yesu kilikuwa muhimu sana? Kwa sababu kadhaa.

Uaminifu wa Yesu hadi kifo ulithibitisha kwamba mwanadamu anaweza kudumisha utimilifu kwa Mungu.

Kifo cha Kristo kiliandaa nafasi kwa wanadamu fulani kutawala pamoja naye mbinguni. Isitoshe, kiliwafungulia wengine wengi njia ya kufurahia uzima wa milele kwenye paradiso duniani.

Jioni kabla ya kifo chake, Yesu alitumia mkate usiotiwa chachu na divai nyekundu kama mifano ya dhabihu yake yenye upendo akiwa mwanadamu. Naye aliwaambia wanafunzi wake: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (Luka 22:19) Je, wewe utakumbuka tukio hilo muhimu?

Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ujiunge nao katika kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu. Mwaka huu tarehe ya ukumbusho huo ni Jumatano, Aprili 12, baada ya jua kushuka. Unaweza kuhudhuria mwadhimisho huo katika Jumba la Ufalme lililo karibu nawe. Waulize Mashahidi wa Yehova walio karibu nawe saa na mahali hususa.