Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Furaha ya Familia—Unaweza Kuipata?

Furaha ya Familia—Unaweza Kuipata?

Furaha ya Familia—Unaweza Kuipata?

Mwaka uliopita, mama mmoja kijana aliandika barua kwa ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Mexico na kuomba msaada ili familia yake iwe na furaha. Alieleza kwamba alifurahia kusoma gazeti Amkeni! Alisema hivi:

“Niliolewa miaka mitatu iliyopita nami ningependa kupata mashauri na mapendekezo ya jinsi ninavyoweza kuwa na familia nzuri. Mimi na mume wangu tulipata mvulana mrembo miaka miwili iliyopita nami ningependa pia kumlea vizuri.”

Mama huyo alipata habari kuhusu kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia naye akaandika akiomba nakala. Watu wengine wengi wamefanya hivyo pia. Baada ya kukisoma wengi wameeleza jinsi kilivyowasaidia. Kati ya sura zenye kupendeza za kitabu hicho ni “Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana,” “Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu,” na “Dumisha Amani Nyumbani Mwako.”

Unaweza kuomba kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia bila malipo.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.