Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je Mungu Anajali?

Je Mungu Anajali?

Je Mungu Anajali?

Watu wengi husema kwamba mungu angekuwako, hangewaruhusu wanadamu wateseke sana. Kwa kawaida watu fulani huuliza, “Mungu alikuwa wapi tulipomhitaji?” Kwa muda mrefu mamilioni ya watu wametaabika sana, wengine hata wameteswa vibaya hadi kifo.

Wakati huohuo, utaratibu wa ajabu na ubuni wa vitu hai unaonyesha waziwazi kwamba kuna muumba anayejali. Lakini Mungu anayetujali angewezaje kuruhusu tuteseke sana? Ili tumwabudu Mungu kwa njia inayofaa, ni lazima tupate jibu lenye kuridhisha la swali hilo muhimu. Tutalipata wapi?

Tunakutia moyo upate nakala yako ya broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? Tunaamini kwamba ukichunguza kwa makini sehemu yenye kichwa “Sababu Kwa Nini Mungu Ameruhusu Kuteseka” na ile yenye kichwa “Matokeo ya Uasi Yamekuwa Nini?” utapata majibu yenye kuridhisha.

Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea broshua Je, Kweli Mungu Anakujali? bila masharti.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.