Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mungu Anajali!

Mungu Anajali!

Mungu Anajali!

NJIA ya Mungu ya kushughulikia uasi ulioanza Edeni inatuonyesha upendo wake kwa ajili ya kila mmoja wetu na jinsi anavyopendezwa na wakati wetu ujao. Tafadhali chunguza uthibitisho ufuatao kwamba Mungu kwa kweli anatujali, na usome maandiko yaliyoonyeshwa katika Biblia yako.

❖ Ametupa dunia iliyojaa umaridadi wa kiasili, wanyama wenye kuvutia, na nchi yenye kutokeza chakula.—Matendo 14:17; Waroma 1:20.

❖ Ametupa mwili wa ajabu unaotuwezesha kufurahia mambo mbalimbali kila siku, kama vile kuonja chakula kitamu, kuona machweo, kusikia mtoto akicheka, na kuhisi mpendwa wetu akitugusa kwa wororo.—Zaburi 139:14.

❖ Yeye hutuandalia mwongozo wenye hekima unaotusaidia kukabiliana na matatizo na mikazo.—Zaburi 19:7, 8; 119:105; Isaya 48:17, 18.

❖ Anatupa tumaini lenye kupendeza, kutia ndani tazamio la kuishi katika paradiso duniani na kuona ufufuo wa wapendwa wetu waliokufa.—Luka 23:43; Yohana 5:28, 29.

❖ Alimtuma Mwana wake mzaliwa pekee afe kwa ajili yetu ili tuwe na tumaini la kuishi milele.—Yohana 3:16.

❖ Amesimamisha Ufalme wa Kimasihi mbinguni na kutupatia uthibitisho wa kutosha kwamba Ufalme huo utaongoza mambo yote duniani.—Isaya 9:6, 7; Mathayo 24:3, 4, 7; Ufunuo 11:15; 12:10.

❖ Anatualika tusali, tumimine mahangaiko yetu ya moyoni, na tunapofanya hivyo yeye husikiliza kwa makini.—Zaburi 62:8; 1 Yohana 5:14, 15.

❖ Tena na tena yeye huwahakikishia wanadamu upendo wake mwingi na kwamba anawajali.—1 Yohana 4:9, 10, 19.