Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ndoa Yao Iliokolewa

Ndoa Yao Iliokolewa

Ndoa Yao Iliokolewa

Mwajiri mmoja huko Afrika Kusini aligundua kwamba mfanyakazi wake mmoja aitwaye Bella, alikuwa na matatizo katika ndoa yake. Hivyo, mwajiri huyo akamwomba Thandi ambaye ni Shahidi wa Yehova azungumze na Bella. Bella alimwambia Thandi kwamba alikuwa ameamua kumtaliki mume wake.

Thandi alimpa Bella vitabu viwili vya Siri ya Kupata Furaha ya Familia na akamtia moyo ampe mume wake kitabu kimoja. Bella alifanya hivyo. Baada ya juma moja, Bella alimwambia Thandi kwamba mume wake alikuwa akikisoma kitabu hicho na hali ya familia yao ilikuwa imeanza kubadilika na kuwa bora. Baada ya miezi mitatu, Bella alimwambia Thandi kwamba Mungu ameiokoa ndoa yao kupitia sala na kitabu Furaha ya Familia. Hata hivyo, huo haukuwa mwisho wa jambo hilo.

Mwajiri wa Bella aliposikia kilichotokea, alipendekeza kwamba kila mfanyakazi apewe kitabu hicho. Hatimaye zaidi ya nakala 100 za kitabu Furaha ya Familia, chenye kurasa 192, zilitolewa kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo. Kati ya sura zinazovutia za kitabu hicho ni “Ikiwa Ndoa Imo Katika Hatua ya Kuvunjika,” “Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu,” na “Dumisha Amani Nyumbani Mwako.”

Unaweza kuomba kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia bila masharti.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.