Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tukio Ambalo Hupaswi Kulikosa

Tukio Ambalo Hupaswi Kulikosa

Tukio Ambalo Hupaswi Kulikosa

“Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” Yesu Kristo, Bwana wetu alisema maneno hayo ambayo yanapatikana kwenye Luka 22:19, alipoanzisha Ukumbusho wa kifo chake. Ni kifo cha Yesu ambacho kiliwafungulia wanadamu tumaini la kupata uzima wa milele katika Paradiso. Hivyo tunapaswa kukumbuka kifo chake.

Je, utahudhuria Ukumbusho huo mwaka huu?

Tafadhali, pokea mwaliko huu kutoka kwa Mashahidi wa Yehova na ujiunge nao katika kuadhimisha tukio hilo muhimu. Mwadhimisho huo utakuwa baada ya jua kushuka katika tarehe inayolingana na Nisani 14 kwenye kalenda ya Biblia. Mwaka huu tarehe ya ukumbusho huo ni Jumatatu, Aprili 2. Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu wanaweza kukuambia mahali na saa ambayo tukio hilo litafanyika.