Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, mtu huyu ananifaa?

Je, mtu huyu ananifaa?

Vijana Huuliza . . .

Je, mtu huyu ananifaa?

Jibu maswali yafuatayo:

Ungetaka mtu ambaye atakuwa mwenzi wako awe na sifa gani? Katika orodha ifuatayo weka alama ya ✔ kando ya sifa nne unazoona kuwa muhimu zaidi.

․․․․․․․․ mwenye sura nzuri ․․․․․․․․ anayethamini mambo ya kiroho

․․․․․․․․ mwenye urafiki ․․․․․․․․ mwenye kutegemeka

․․․․․․․․ maarufu ․․․․․․․․ mwenye maadili yanayofaa

․․․․․․․․ mcheshi ․․․․․․․․ mwenye miradi inayofaa

Ulipokuwa mdogo ulimpenda mtu fulani? Kwenye orodha juu weka alama ya X kando ya sifa uliyopendezwa nayo zaidi kwa mtu huyo wakati huo.

HAKUNA sifa yoyote mbaya kati ya hizo zilizotajwa hapo juu. Kila moja inavutia kwa njia fulani. Hata hivyo, si ni kweli kwamba ukiwa kijana unavutiwa zaidi na mtu aliye na sifa kama zile zilizo kwenye safu ya kushoto?

Lakini unapoendelea kukomaa, unaanza kutumia nguvu zako za ufahamu kuchunguza mambo mazito zaidi, kama yale yaliyo kwenye safu ya kulia. Kwa mfano, unaanza kutambua kwamba huenda msichana mrembo zaidi katika mtaa wenu si mwaminifu au huenda mvulana maarufu zaidi darasani hana maadili yanayofaa. Ikiwa “umepita upeo wa ujana,” wakati wa maisha ambapo hamu ya ngono huanza kuwa yenye nguvu, huenda ukaangalia zaidi ya sifa za nje ili kujibu swali hili, Je, mtu huyu ananifaa?—1 Wakorintho 7:36.

Je, Mtu Yeyote Tu Atafaa?

Kadiri wakati unavyopita, huenda ukavutiwa na watu kadhaa wa jinsia tofauti. Lakini si mtu yeyote tu atakayekufaa. Ukweli ni kwamba unatafuta mwenzi wa kudumu, ambaye atakuza sifa zako bora na ambaye wewe pia utamchochea kufanya hivyo. (Mathayo 19:4-6) Mtu huyo anaweza kuwa nani? Lakini kabla ya kujibu swali hilo, unahitaji ‘kutazama kioo’ na kujichunguza kwa unyoofu.—Yakobo 1:23-25.

Ili uweze kujichunguza, jibu maswali yafuatayo:

Nina sifa gani nzuri?

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

Nina udhaifu gani?

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

Nina mahitaji gani ya kihisia na ya kiroho?

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

Kujichunguza mwenyewe si jambo rahisi, lakini maswali kama hayo yanaweza kukusaidia. * Kadiri unavyojielewa, ndivyo utakavyoweza kumpata mtu atakayekusaidia kukuza sifa zako nzuri badala ya udhaifu wako. Lakini vipi ikiwa unafikiri umempata mtu anayekufaa?

Je, Uhusiano Utafanikiwa?

Ili kujibu swali hilo, mchunguze rafiki yako kwa makini. Lakini uwe mwangalifu! Huenda ukapendezwa kuona tu kile unachotaka kuona. Hivyo usiwe na haraka. Jaribu kutambua utu halisi wa rafiki yako.

Wengi ambao huchumbiana huchunguza mambo kijuujuu tu. Wao hukazia fikira mambo wanayopatana: ‘Tunapenda aina ileile ya muziki.’ ‘Tunapenda kufanya mambo yaleyale.’ ‘Sisi hukubaliana kuhusu kila kitu!’ Hata hivyo, kama ilivyotajwa awali, ikiwa umepita upeo wa ujana, hutachunguza mambo kijuujuu tu. Unahitaji kutambua “mtu wa siri wa moyoni.”—1 Petro 3:4; Waefeso 3:16.

Kwa mfano, badala ya kukazia hasa mambo mnayokubaliana, ni vizuri kuzingatia kinachotokea wakati ambapo hamkubaliani. Kwa maneno mengine anasuluhishaje ugomvi? Je, ni kwa kusisitiza njia yake tu, labda kwa ‘kulipuka kwa hasira’ au kwa “matukano”? (Wagalatia 5:19, 20; Wakolosai 3:8) Au je, mtu huyo anakubali sababu, yaani, yuko tayari kuachilia jambo ili kuendeleza amani ikiwa hakuna kanuni inayovunjwa?—Yakobo 3:17.

Jambo lingine unalopaswa kufikiria ni: Je, mtu huyo anapenda kukuongoza, kukusimamia katika kila jambo, au ni mwenye wivu? Je, anataka kujua kila kitu unachofanya? Msichana mmoja anayeitwa Nicole anasema hivi: “Ikiwa mtu anataka kukudhibiti katika kila jambo au ana wivu, basi ujue kuna tatizo kubwa. Mimi husikia kuhusu watu wanaochumbiana ambao hupigana kwa sababu mmoja anajihisi vibaya kwa sababu mwenzake hapigi simu na kumweleza mahali alipo. Ninafikiri hiyo ni dalili mbaya.”

Wengine wana maoni gani kuhusu rafiki yako? Huenda ukapenda kuzungumza na watu ambao wamemfahamu kwa muda fulani, kama vile watu wakomavu katika kutaniko lake. Watakuambia ikiwa mtu huyo ‘anashuhudiwa vema.’—Matendo 16:1, 2. *

Je, Unapaswa Kuvunja Uhusiano?

Lakini vipi ukitambua kwamba mtu ambaye umekuwa na urafiki wa karibu naye hawezi kuwa mwenzi mzuri wa ndoa? Ikiwa ndivyo, huenda ikafaa kukatiza uhusiano huo. Biblia inasema: “Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha.”—Methali 22:3. *

Baada ya muda, huenda utaingia katika uhusiano mpya. Ikiwa ndivyo, bila shaka utakuwa na mtazamo uliosawazika, mtazamo ambao umeupata kupitia uzoefu. Huenda wakati huo ukijiuliza: “Je, mtu huyu ananifaa?” utajibu ndiyo!

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 24 Ili kupata maswali mengine ya kujiuliza, ona ukurasa wa 30 wa Amkeni! ya Januari 2007.

^ fu. 30 Ona pia maswali katika sanduku kwenye ukurasa wa 19-20.

^ fu. 32 Kwa habari zaidi kuhusu kuvunja uhusiano, ona Amkeni! la Machi 22, 2001 (22/3/2001), ukurasa wa 12-14.

MAMBO YA KUFIKIRIA

▪ Una sifa gani nzuri zitakazokufanya uwe mwenzi mzuri wa ndoa?

▪ Ungependa mwenzi wako wa ndoa awe na sifa gani?

▪ Ni katika njia zipi unaweza kujifunza mengi kuhusu tabia, mwenendo, na sifa za mtu ambaye umeanzisha uhusiano wa karibu naye?

[Sanduku katika ukurasa wa 19]

Je, anaweza kuwa mume anayefaa?

MAMBO MUHIMU

❑ Anatumiaje mamlaka yoyote anayopewa?—Mathayo 20:25, 26.

❑ Ana miradi gani?—1 Timotheo 4:15.

❑ Je, anajaribu kufikia miradi hiyo?—1 Wakorintho 9:26, 27.

❑ Ana marafiki wa aina gani?—Methali 13:20.

❑ Mtazamo wake kuelekea fedha ukoje?—Waebrania 13:5, 6.

❑ Anapendezwa na burudani za aina gani?—Zaburi 97:10.

❑ Mavazi yake yanaonyesha kuwa yeye ni mtu wa aina gani?—2 Wakorintho 6:3.

❑ Anaonyeshaje upendo wake kwa Yehova?—1 Yohana 5:3.

SIFA NYINGINE

❑ Je, anafanya kazi kwa bidii?—Methali 6:9-11.

❑ Je, anajua kutumia fedha vizuri?—Luka 14:28.

❑ Je, wengine wanasema ana sifa nzuri?—Matendo 16:1, 2.

❑ Je, anawaheshimu wazazi wake?—Kutoka 20:12.

❑ Je, anawajali wengine?—Wafilipi 2:4.

ISHARA MBAYA

❑ Je, yeye hukasirika upesi?—Methali 22:24.

❑ Je, anajaribu kukuingiza katika ukosefu wa maadili katika ngono?—Wagalatia 5:19.

❑ Je, yeye huwapiga wengine au kuwatukana?—Waefeso 4:31.

❑ Je, ni lazima atumie kileo ili afurahi?—Methali 20:1.

❑ Je, ana wivu na ubinafsi?—1 Wakorintho 13:4, 5.

[Sanduku katika ukurasa wa 20]

Je, anaweza kuwa mke anayefaa?

MAMBO MUHIMU

❑ Yeye huonyeshaje kwamba anajitiisha katika familia na kutanikoni?—Waefeso 5:21, 22.

❑ Mavazi yake yanaonyesha kuwa yeye ni mtu wa aina gani? —1 Petro 3:3, 4.

❑ Ana marafiki wa aina gani?—Methali 13:20.

❑ Mtazamo wake kuelekea fedha ukoje?—1 Yohana 2:15-17.

❑ Ana miradi gani?—1 Timotheo 4:15.

❑ Je, anajaribu kufikia miradi hiyo?—1 Wakorintho 9:26, 27.

❑ Anapendezwa na burudani za aina gani?—Zaburi 97:10.

❑ Anaonyeshaje upendo wake kwa Yehova?—1 Yohana 5:3.

SIFA NYINGINE

❑ Je, anafanya kazi kwa bidii?—Methali 31:17, 19, 21, 22, 27.

❑ Je, anajua kutumia fedha vizuri?—Methali 31:16, 18.

❑ Je, wengine wanasema ana sifa nzuri?—Ruthu 4:11.

❑ Je, anawaheshimu wazazi wake?—Kutoka 20:12.

❑ Je, anawajali wengine?—Methali 31:20.

ISHARA MBAYA

❑ Je, yeye ni mbishi?—Methali 21:19.

❑ Je, anajaribu kukuingiza katika ukosefu wa maadili katika ngono? —Wagalatia 5:19.

❑ Je, yeye huwapiga wengine au kuwatukana?—Waefeso 4:31.

❑ Je, ni lazima atumie kileo ili afurahi?—Methali 20:1.

❑ Je, ana wivu na ubinafsi? —1 Wakorintho 13:4, 5.